PICHA YETU YA LEO IKIWA NA MSEMO WA KIHAYA WENYE BUSARA NA MAANA KUBWA NDANI YAKE
Kupitia picha yetu ya leo bukobawadau blog tunaendelea
kuwaomba ushirikiano wa kimawazo,pia tusaidiane kuwaelewesha ndugu zetu wengine
kuitembelea blog yetu na mwenye uwezo tunaomba atusaidie vitendea kazi,na ili
tuendele zaidi tupatieni matangazo yenu tuweze tuboresha utendaji
wetu!!!. Chanzo. BukobaMdau Blog
CAMERA YETU NDANI YA HOSPITALI YA MKOA
Camera yetu
inaangaza Hospitali ya Mkoa wa Kagera, Mkoa wenye jumla ya vituo vya kutolea
huduma za afya 246, zikiwemo hospitali 13, Vituo vya afya 23na zahanati
210.
Inaonyesha huduma zinaendelea kama kawaida na hali ya mazingira si
mbaya kabisa na kwa kupitia tovuti ya Mkoa inaseme; MKOA wa Kagera kama ilivyo
mikoa mingine ya Tanzania unaendelea kutoa ... Huduma kwa Watoto yatima
na wanaoishi kwenye mazingira hatarishi .... wazee wanaofika hasa
katika Hospitali hii ya mkoa
Jitiada zetu
za kuonana moja kwa moja na Idara zinayotoa huduma katika hospital
yetu
kuanzia
Utawala, usimamizi mpaka idara ya ODP kwa wagonjwa wa nje hazikufanikiwa ndipo
bukobawadau tukaendelea kufanya kile kinachoweza kuonekana kwa siku ya
leo.
Camera yetu
inaangaza kwa kina na kuona hali halisi ndani ya wodi maalumu ya akinamama
wajawazito kama inavyoonyesha wengine ulazimika kulala chini.
Hapa swali
moja tunaendelea nalo tatizo ni wodi za kulaza wagonjwa hama tatizo ni
vitanda...?!
Tathmini ya
haraka haraka inaonyesha katika mkoa wetu wa Kagera asilimia 90 ya hospitali
zinazotoa huduma ya TIBA ni za taasisi za dini ikilinganisha na Serikali yenye
hospitali moja tu ambayo ni hii ya mkoa
iliyopo mjini hapa!!!
SHEREHE ZA KULITABARUKU KANISA KATOLIKI JIMBO LA BUKOBA MJINI BAADA YA UKARABATI MKUBWA ULIOCHUKUA MIAKA 17 KUFANYIKA 7/10/2012 NA MAZISHI YA MAREHEMU MWADHAMA KARDINAL RUGAMBWA NI 6/10/2012
Shughuli ya kuzika masalia ya mwili wa Mwadhama
Kardinali Laurean Rugambwa ambaye alikuwa Kardinali wa kwanza mwafrika
itafanyika rasmi katika Kanisa la Jimbo Katoliki la Bukoba tarehe 6/10/2012
ikiwa ni miaka 15 tangu alipozikwa kwa muda katika kanisa la Kashozi.
Tarehe 7/10 /2012 kutafanyika sherehe za kulitabaruku Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Mjini baada ya ukarabati mkubwa uliochukua miaka 17.Shughuli ya kuzikwa upya kwa masalia ya Marehemu Kardinali Rugambwa itakwenda sambamba na sherehe za kuadhimisha miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.
Mwadhama Laurean Kardinali Rugambwa,aliyekuwa Kardinali wa kwanza Mtanzania na Mwafrika alifariki dunia 8/12/1997 na kuzikwa tarehe 17/12/1997 kwa muda katika Kanisa Katoliki lililopo Kashozi Wilaya ya Bukoba Vijijini kutokana na ukarabati uliokuwepo katika kanisa hili pichani na sasa unakamili ni Kanisa la Jimbo Katoliki Bukoba.
Marehemu Mwadhama Kardinali Laurean Rugambwa alizaliwa tarehe 12/7/1912 katika eneola Rutabo Kamachumu Wilaya ya Mulebwa na alikuwa Padri 12/12/1947 na aliteuliwa kuwa Kardinali 23/3/1960.
Tarehe 7/10 /2012 kutafanyika sherehe za kulitabaruku Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Mjini baada ya ukarabati mkubwa uliochukua miaka 17.Shughuli ya kuzikwa upya kwa masalia ya Marehemu Kardinali Rugambwa itakwenda sambamba na sherehe za kuadhimisha miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.
Mwadhama Laurean Kardinali Rugambwa,aliyekuwa Kardinali wa kwanza Mtanzania na Mwafrika alifariki dunia 8/12/1997 na kuzikwa tarehe 17/12/1997 kwa muda katika Kanisa Katoliki lililopo Kashozi Wilaya ya Bukoba Vijijini kutokana na ukarabati uliokuwepo katika kanisa hili pichani na sasa unakamili ni Kanisa la Jimbo Katoliki Bukoba.
Marehemu Mwadhama Kardinali Laurean Rugambwa alizaliwa tarehe 12/7/1912 katika eneola Rutabo Kamachumu Wilaya ya Mulebwa na alikuwa Padri 12/12/1947 na aliteuliwa kuwa Kardinali 23/3/1960.
Shughuli hizi zinatarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi
ya 10,000 kutoka nje ya Bukoba,viongozi mbalimbali pamoja na maaskofu kutoka
Ulaya,Kenya,Uganda, Burundi, na mabalozi mbalimbali na viongozi wakuu wa nchi ni
sehemu ya Waalikwa!!.
HEKAHEKA ZA HAPA NA PALE BARABARA YA KASHOZI
Hii ni barabara ya kashozi inayokutana na
barabara ya kashai ,ni barabara yenye mkusanyiko wa watu wengi ,shughuli nyingi
na magari mengi na umaharufu wa barabara hii unazidi kuwepo siku
hadi siku ukizingatia ndipo utakapo pita mwili wa Marehemu Cardinal Laurean Rugambwa kutoka parokia ya Kashozi
ulipozikwa kwa muda,na kuletwa katika kanisa la jimbo katoliki bukoba, tukio
linaloenda kuchukua kasi na kuandika historia mpya katika ukanda huu
litakalofanyika tarehe 6/10/2012.Ikiwa ni miaka 15 tangu alipozikwa kwa
muda.
Ni barabara moja tegemezi kwa wakazi wa Kashai NHC,kashai halisi ,kilimanjaro,Kisindi,Mafumbo, Kashai Matopeni , Buhembe,kyabitembe, Kahororo, Nyanshenye usawa wa Nyamkazi na vitongoji kadha wakadha...!
Barabara hii nje ya kuwa na shughuli nyingi za kijamii viwanda vya mbao, kiwanda cha samaki cha vic fish,kiwanda cha maji asilia,maghala mbalimbali ya vyakula,Soda na Bia,mashine za kusaga na kukoboa, ,pia inauwelekeo wa shule nyingi za msingi na sekondari.
Pitapita za hapa na pale barabara ya Kashozi.
Sehemu ya raia kuvukia (zebra line)nilichokiona hapa bado watu wanatakiwa kuelimishwa juu ya matumizi yake.
Ni barabara moja tegemezi kwa wakazi wa Kashai NHC,kashai halisi ,kilimanjaro,Kisindi,Mafumbo, Kashai Matopeni , Buhembe,kyabitembe, Kahororo, Nyanshenye usawa wa Nyamkazi na vitongoji kadha wakadha...!
Barabara hii nje ya kuwa na shughuli nyingi za kijamii viwanda vya mbao, kiwanda cha samaki cha vic fish,kiwanda cha maji asilia,maghala mbalimbali ya vyakula,Soda na Bia,mashine za kusaga na kukoboa, ,pia inauwelekeo wa shule nyingi za msingi na sekondari.
Pitapita za hapa na pale barabara ya Kashozi.
Sehemu ya raia kuvukia (zebra line)nilichokiona hapa bado watu wanatakiwa kuelimishwa juu ya matumizi yake.
Comments