Balozi wa Marekani Bw Alfonso Lenhardt akisalimiana na maafisa wa jeshi la wanamaji Tanzania -NAVY.
Mkuu
wa Mipango na Maendeleo(JWTZ) Maj. Gen. Le Mndeme akikata Utepe
akishuhudiwa na Balozi wa Marekani Bw. Alfonso E. Lenhardt, kushoto
Kamanda mkuu kikosi cha wanamaji NAVY Maj.Gen. Said Shaban Omary.
Balozi wa Marekani Bw.Alfonso Lenhardt akihutubia wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.
Meneja wa programu US Navy Bw.Steve Poland akikabidhi vyeti mmoja kati wahitimu wa mafunzo.
Sehemu ya meza kuu ikiwa na baadhi ya makamanda wa jeshi la marekani na Tanzani
--
Serikali
ya Marekani imetoa msaada wa kuimarisha Mfumo wa Ulinzi baharini wenye
thamani ya dola za Marekani milioni 1 ikiwa ni mafunzo pamoja na vifaa.
Balozi
wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt ameshiriki katika hafla ya
kukata utepe wa kufungua mafunzo pamoja na msaada huo katika kambi ya
Kigamboni Wanamaji ya Kigamboni ya TPDF jijini Dar es Salaam.
Msaada
huo kwa ujumla utasaidia ushirikiano wa kupata taarifa miongoni mwa
Mamlaka za Bandari, askari wa majini na Jeshi la Wananchi wa Tanzania
ikiwa ni kuongeza usalama majini.
Comments