Siku Ya Mtanzania


Mahali: Tanzania House, 1232 22Nd Street, N.W. Washington D.C.; 20037Tarehe: SEPTEMBA 15, 2012 Kiingilio: BUREMuda: (Saa 4:00 asubuhi – Saa 12 Jioni)Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Washington D.C. unawakaribisha Watanzania wote waishio maeneo ya DMV (District of Columbia, Maryland na Virginia) na vitongoji vyake, kuhudhuria siku ya Mtanzania, ambapo Watanzania watashirikikwenye kuonyesha bidhaa, tamaduni, mila na desturi za Kitanzania kwa wageni (Wamarekani na wa Mataifa mengine) watakaotembelea ubalozini.


Madhumuni makuu ya Ubalozi kuandaa Siku ya Mtanzania kwanza ni kuwaelimisha wenyeji wa Marekani kuhusu Tanzania. Pili kuitangaza zaidi Tanzania kwa kuvutia watalii wengi kutembelea Tanzania. Tatu ni kutambulisha na kutangaza biashara mbalimbali na hudumazitolewazo na Watanzania waishio hapa Marekani.

Ubalozi unaomba Watanzania wenye bidhaa mbambali za Kitanzania, mapishi (wenye leseni),vikundi vya ngoma, muziki, mitindo, na Watanzania wenye kampuni za utalii, kujiandikisha ubalozini kuanzia tarehe 1 hadi 15 Agosti, 2012 kwa maandalizi ya siku hiyo.

Kwa Watanzania watakaopenda kujitolea kushiriki siku hiyo au kuonyesha bidhaa mbalimbali wajiandikishe kwa wafuatao:

Dkt. Suitbert Mkama 202 884 1087 au barua pepe smkama@tanzaniaembassy-us.orgAsia Dachi 202 884 1096 barua pepe adachi@tanzaniaembassy-us.org Rosemary Mziray 202 884 1081 au barua pepe rmziray@tanzaniaembassy-us.org Ubalozi unapenda kuwahamasisha Watanzania kuvaa vazi la Kitanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.