SIMBA NA YANGA KUCHEZA USIKU TAIFA OKTOBA 3 LIVE SUPER SPORT DUNIA NZIMA
Simba SC |
Na Prince
Akbar
MECHI ya
kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya watani wa jadi, Simba na
Yanga itakayopigwa Oktoba 3, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachezwa
kuanzia Saa 1:00 usiku na kuonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha
SuperSport.
Ofisa Habari
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura ameiambia BIN
ZUBEIRY leo kwamba hiyo itakuwa moja kati ya mechi tano za Ligi Kuu
zilizobatizwa jina Super Weekend katika mzunguko wa kwanza, ambazo zote
zitaonyeshwa moja kwa moja na SuperSport, zikianza kati ya saa 1:30 jioni na saa
1:00 usiku.
Mechi
nyingine ni za Septemba 28 mwaka huu kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku, Simba na Tanzania Prisons
Septemba 29 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11:00 jioni, Yanga na
African Lyon Septemba 30, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11:00 na
Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar Oktoba 1, Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam
kuanzia saa 10:30 jioni.
Yanga SC |
Comments