TFF YAUPONGEZA UONGOZI MPYA IRFA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa (IRFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Septemba 9 mwaka huu) mjini Iringa.
 
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa IRFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Iringa.
 
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya IRFA chini ya uenyekiti wa Cyprian Kuyava ambaye amechaguliwa kuongoza chama hicho kwa mara ya kwanza.
 
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Iringa kwa kuzingatia katiba ya IRFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
 
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya IRFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.
 
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Cyprian Kuyava (Mwenyekiti), Stanford Mwakasala (Makamu Mwenyekiti), Eliud Mvella (Katibu) na John Ambwene (Katibu Msaidizi).
 
Wengine ni Ramadhan Mahano (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Coaster Magoloso (Mwakilishi wa Klabu TFF), Abdallah Kiyumbo (Mhazini), wakati wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Maulid Tofi na David Mwamalekela.
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.