YANGA YATIMUA VIONGOZI WOTE WA KUAJIRIWA, WAMO SENDEU NA MWESIGWA
Sanga akizungumza na Waandishi wa Habari mida hi. kulia ni Tito Osoro, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na kushoto Isaac Chanji, Mjumbe wa kuteuliwa |
Mkutano na Waandishi |
Na
Mahmoud Zubeiry
UONGOZI wa
klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, umeisimamisha kazi Sekretarieti nzima ya klabu,
akiwemo Katibu Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu, kutokana na
kile ilichoeleza utendaji usioridhisha.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari ‘mida hii’ makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es
Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga alisema kwamba maamuzi hayo
yamefuatia kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika tangu saa 5:30 leo hadi
saa 9:30.
Wengine
wanaokumbwa na panga hilo ni Masoud Saad, aliyekuwa Ofisa Utawala, Philip
Chifuka aliyekuwa Mhasibu na Hafidh Saleh aliyekuwa Meneja ambaye anahamishiwa
kwenye majukumu mengine.
“Tumesitisha
mikataba ya sekretarieti nzima, pia tumefanya marekebisho, tumemtoa Meneja wa
timu na muda si mrefu tutamtangaza Meneja mwingie pamoja na sekretarieti
mpya,”alisema Sanga.
Aidha, Sanga
alisema Kocha Mbelgiji, Tom Saintfieti anapewa onyo kali kwa kuzungumza ovyo na
vyombo vya habari.
“Tumekwishakutana
naye mara kadhaa kumpa utaratibu wa kuzungumza na vyombo vya habari, sasa
tutamuandikia barua ya kumkumbusha wajibu wake na kuzingatia wajibu wake,
kutozungumza na vyombo vya habari
holela,”alisema.
Kwa ujumla
maamuzi haya yanakuja baada ya Yanga kuanza vibaya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara, ikiambulia pointi moja tu katika mechi zake mbili za awali, kutokana na
sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi
na Jumatano ikachapwa mabao 3-0 Morogoro Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Comments