Akamatwa Na Sehemu Za Siri Za Mpwa Wake A. Kusini




Mwanamume mmoja nchini Afrika Kusini amekamatwa baada ya kupatikana akiwa na sehemu za siri kwenye pochi lake ambazo zinaaminika kuwa za mpwa wake ambaye hajulikani aliko. 

 Msemaji wa polisi, aliambia BBC kuwa babada ya kukamatwa kwake , mwanaume huyo aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye msitu katika mkoa wa Eastern Cape, ambako mwili uliokatwakatwa ulipatikana. 

 Kichwa cha msichana huyo pamoja na miguu yake ilikuwa imekatwa na zilipatikana karibu na kiwiliwili chake. Mtu huyo mwenye umri wa miaka 42, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.

 Mmwanaume huyo alishtakiwa baada ya kushukiwa kuhusika na kutoweka kwa msichana huyo mwenye umri wa miaka 18, aliyepotoea katika mji wa Ngcobo siku ya Jumapili. 

 Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela alisema kuwa sehemu hizo za siri, zilipatikana ndani ya pochi lake. Alisema sababu ya kuuawa kwa msichana huyo haijulikani na kwamba uchunguzi unafanyika.

 Alipoulizwa ikiwa mauaji hayo yanahusishwa na waganga ambapo sehemu za mwili wa watu hutumiwa kwenye madawa yao, bwana Fatyela alisema kuwa hawezi kubaini hilo kwa sasa. Kumekuwa na visa vingi vya kuuza sehemu za siri za watu katika sehemu nyingi za Afrika kwa sababu sawa na hizo.

 Afrika Mashariki imeshuhudia visa vingi vya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi au maalbino, huku sehemu za miili yao zikikatwa kwa sababu za kishirikina. Mwanaume huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.

                                     BBC-SWAHILI

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA