DI MATTEO ATUPIWA VIRAGO CHELSEA

Di Matteo amebaki historia Chelsea

BILIONEA Mrusi Roman Abramovich amemfukuza kazi Kocha Mtaliano, Roberto Di Matteo asubuhi ya leo baada ya matokeo mabaya mfululizo.Kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog
 
Mmiliki huyo wa Chelsea, amekasirishwa na matokeo mabaya ya timu hiyo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, na kumfukuza kazi Mtaliano huyo baada ya timu kuzabwa mabao 3-0 na Juventus jana, ikiwa ni miezi sita tu tangu aipe timu hiyo taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Sasa mtu wa kwanza kabisa ambaye Abramovich anamtaka akarithi mikoba ya Mtaliano huyo ni kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola, na kama akikwama kwa Mspanyola huyo ambaye amesema hataki ukocha tena kwa sasa, basi atahamishia ndoana zake kwa Rafa Benitez.
MAKOCHA WALIODUMU MUDA MFUPI CHESLEA:
Guus Hiddink         Siku 105
Felipe Scolari         Siku 223
Avram Grand          Siku 247
Andre Villas-Boas   Siku 256
Roberto Di Matteo   Siku 262
MATOKEO YALIYOMFUKUZISHA KAZI DI MATTEO:
Oktoba 23: Shakhtar 2 Chelsea 1        (Ligi ya Mabingwa)
Oktoba 28: Chelsea 2 Man United 3    (Ligi Kuu)
Oktoba 31: Chelsea 5 Man United 4    (Kombe la Ligi)
Novemba 3: Swansea 1 Chelsea 1      (Ligi Kuu)
Novemba 7: Chelsea 3 Shakhtar 2      (Ligi ya Mabingwa)
Novemba 11: Chelsea 1 Liverpool 1     (Ligi Kuu)
Novemba 17: West Brom 2 Chelsea 1  (Ligi Kuu)
Novemba 20: Juventus 3 Chelsea 0     (Ligi ya Mabingwa)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*