DJ Too Short” ameibuka mshindi katika shindano la Hannessy DJ Challenge
Balozi
wa kinywaji cha Hennessy Cyrille Auriol na Mwenyekiti wa Makampuni ya
Qweensway Group, Amin Hirjee, wakimzawadia DJ maarufu nchini, DJ Too
Short mkanda wa ushindi katika shindano la Hennessy DJ Challenge
lililofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa Serena Hotel.
Picha: Mpiga Picha wetu
………………………………..
Mwandishi Wetu
DJ Mohamed Ali maarufu kwa jina
la “DJ Too Short” ameibuka mshindi katika shindano la Hannessy DJ
Challenge lililofanyika kwenye ukumbi wa hotel ya Serena jijini.
Ushindi wa DJ Too short
umetokana na jinsi alivyoweza kuwachezesha mashabiki kibao wa kinywaji
cha Hennessy katika usiku maalum kinywaji hicho.
Balozi wa dunia wa Hennessy,
Cyrille Auriol na Mwenyekiti wa makampuni ya Qweensway Group, Amin
Hirjee walimzawadia zawadi ya ushindi DJ huyo.
Kutokana na ushindi huo, DJ Too
Short anakuwa Mtanzania wa kwanza kushinda nafasi hiyo na kuzawadiwa
mkanda wa utambulisho wake na yeye kushukuru kwa mafanikio hayo.
Mbali ya tukio hilo, Balozi Auriol alikutana na wadau mbali mbali wakiwemo wafanyabiashara na wadau wa masuala ya maonyesho ya mavazi (modal) au walimbwende na kujadili changamoto mbali mbali zinazowakabili hasa wafanyabiashara wa vinywaji.
Mbali ya tukio hilo, Balozi Auriol alikutana na wadau mbali mbali wakiwemo wafanyabiashara na wadau wa masuala ya maonyesho ya mavazi (modal) au walimbwende na kujadili changamoto mbali mbali zinazowakabili hasa wafanyabiashara wa vinywaji.
Balozi huyo alifanya ziara yake ya
siku mbili, ikiwa ni miongoni mwa ziara yake ya siku tano katika nchi
za Afrika Mashariki. Hii ni mara ya pili kutembelea Tanzania.
Alisema kuwa biashara ya vinywaji ambayo inawahusu wafanyabiashara, wanamuziki na sekta nyingine kwa sasa inakuwa kwa kasi pamoja na kuwepo kwa changamoto mbali mbali.
Alisema kuwa biashara ya vinywaji ambayo inawahusu wafanyabiashara, wanamuziki na sekta nyingine kwa sasa inakuwa kwa kasi pamoja na kuwepo kwa changamoto mbali mbali.
Alisema kuwa wanajitahidi kuondoa
changamoto hizo na nyingi zinatokana na ushindani katika soko husika na
moja ya mikakati yao ni kuwafundisha watoa huduma hiyo ili kuweza
kufikia kiwango cha kimataifa. KWA HISANI YA FULLSHANGWE BLOG
Comments