FERGUSON APANIA MABAO 100 LIGI KUU ENGLAND

Rekodi ya karibu kwa Fergie kufikisha idadi hiyo akiwa na United ilikuwa ni msimu wa 1999/2000, wakati Mashetani Wekundu walipofunga jumla ya mabao 97 na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa tofauti ya pointi 18 dhidi ya Arsenal

 MANCHESTER, England

KOCHA Sir Alex Ferguson, ameshawikika kuamini kuwa, kikosi chake cha Manchester United kitafanya makubwa msimu huu wa Ligi Kuu, ikiwamo kutikisa nyavu mara 100 katika mechi tofauti za ligi hiyo.
Rekodi ya karibu kwa Fergie kufikisha idadi hiyo ilikuwa ni msimu wa 1999/2000, wakati Mashetani Wekundu walipofunga jumla ya mabao 97 na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa tofauti ya pointi 18 dhidi ya Arsenal.
Tambo za Fergie msimu huu zimekuja wakati klabu hiyo ikiwa imefunga mabao kadhaa kupitia wachezaji 13 tofauti, huku Robin van Persie akiongoza kwa mabao yake 11 katika mechi 14 za mashindano tofauti.
Mabao manane ya Mholanzi huyo katika mechi nane alizoanzishwa katika Ligi Kuu, yameifanya Man United kufunga jumla ya mabao 26 - kabla ya pambano lao la jana Jumamosi dhidi ya Aston Villa kwenye Uwanja wa Villa Park.
Fergie anasisitiza kuwa, kikosi chake kina uwezo wa kuimarika kila uchao na kuwezesha kufunga mara tatu zaidi ya hayo.
Akasema kuwa: “Jambo la kufarahisha kwangu ni kuzidi kutikisa nyavu zaidi na zaidi kwa kila timu itakayokatiza mbele yetu. Kuwa na wafungaji tofauti 13 hadi sasa, ni jambo linalotupa nguvu ya ziada katika mechi zetu.
“Tuna mabeki kama Evans na Evra ambao tayari wameshafunga mabao mawili kila mmoja na kuwa mara mbili zaidi ki-utendaji wao. Lakini pia tutapata kutoka kwa kila mmoja miongoni mwao ama mwingine,” alisema Fe

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI