JK atuma rambirambi kwa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mshahamu Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa,
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumanne, Novemba 6, 2012, amelitumia Kanisa Katoliki Tanzania salamu za
rambirambi kuomboleza kifo cha Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Mhashamu
Baba Askofu Aloysius Balina aliyefariki dunia majira ya saa tano asubuhi leo
kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza.
Katika
salamu zake za rambirambi kwa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mshahamu Baba
Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mshtuko mkubwa
taarifa za kifo cha Mhashamu Baba Askofu Aloysius Balina ambaye nimeambiwa
ameaga dunia asubuhi ya leo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Buganda,
Mwanza, kwa ugonjwa wa kansa.”
Amesema
Rais Kikwete katika salamu zake hizo: “Mhashamu Baba Askofu Balina alikuwa
kiongozi hodari na mwadilifu ambaye siyo tu alichangia kipekee katika mwenendo mzuri
wa kiroho wa waumini wa Kanisa Katoliki bali pia katika maendeleo ya Watanzania
wote kwa jumla.”
“Kifo
chake kimetuondolea kiongozi mwema ambaye tutazikosa busara zake na uongozi
wake. Lakini napenda kukuhakishia Mshahamu Baba Askofu kuwa sisi ndani ya
Serikali tutaendelea kutambua na kuthamini mchango wa Askofu Balina alioutoa
kwa nchi yetu katika maisha yake,” amesema Rais Kikwete na
kuongeza:
“Baba
Askofu, nakuomba upokee salamu za rambirambi za Serikali ninayoiongoza na zangu
binafsi kufuatia msiba huu mkubwa. Aidha, kupitia kwako, naomba uwafikishie
salamu zangu viongozi na waumini wote wa Kanisa Katoliki kwa kuondokewa na
kiongozi na muumini mwenzao. Naungana nanyi kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa
Rehema, aiweka pema peponi roho ya Marehemu. Amen.”
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6
Novemba, 2012
Comments