Benny Kisaka

Na Mahmoud Zubeiry
MWENYEKITI wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Abbas Pinto amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwakilishi wa Klabu katika uchgauzi wa Chama cha Soka Dar es Salaam.
Juma Pinto
Winga huyo wa timu ya mkoa wa Dar es Salaam, Mzizima United iliyoshiriki Kombe la Taifa, Taifa Cup mwaka 1997 mkoani Kagera, kwa kuchukua fomu ya kuomba nafasi hiyo, ina maana atachuana na Mkurugenzi wa kampuni ya Jambo Concepts Limited, Benny Kisaka, ambaye pia ni Mwana Habari.
Wagombea wengine katika nafasi hiyo ni Philemon Ntahilaja na Frank Mchaki, wakati wanaowania Ujumbe wa Mkutano Mkuu ni Isaac Mazule, Shufaa Jumanne, Shaffi Dauda na Muhisn Balhabou, huku Shaaban Mohamed, Andrew Tupa, Siza Abdallah Chenje, Sunday Mwanahewa, George Wakuganda na Lameck Nyambaya wakiwania Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.
Wanaowania Uenyekiti ni Ahmad Seif Hemed ambaye anachuana na Brown Ernest, Salum Mkemi, Evans Aveva, Ayoub Nyenzi, Juma Jabir na Meba Ramadhan, wakati nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Ally Mayay na Salum Mwaking’inda, na Ukatibu Mkuu, Said Tuliy na Hamisi Ambari ndio waliojiotokeza hadi sasa, ingawa kuna habari Rahim Kangezi ‘Zamunda’ naye atachukau fomu.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika Desemba 8, mwaka huu na fomu za kugombea nafasi mbalimbali zilianza kutolewa tangu Oktoba 29, wakati Novemba 4 hadi 8, Kamati ya Uchaguzi, chini ya Mwenyekiti wake, Juma Simba itapitia fomu za walioomba uongozi.
Novemba 9 hadi 13 utakuwa muda wa pingamizi kwa wagombea, ambazo zitajadiliwa Novemba 14 hadi 16, wakati Novemba 17 hadi 19 watatoa fursa ya kukata rufaa, ambazo zitasikilziwa Novemba 20 hadi 24 na baada ya hapo, Novemba 25 yatatangazwa majina ya wagombea waliopitishwa.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika siku chache tu kabla ya uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.Kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI