KUELEKEA KRISMAS NA MWAKA MPYA, SUMATRA YAAPA KUSHUGHULIKIA KIKAMILIFU WENEYE MABASI YATAKAYOPANDISHA NAULI HOVYO



DAR ES SALAAM, TANZANIA
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imepia mkwara ikisema itawakamata wamiliki wa magari watakaohusika katika kupandisha nauli hovyo wakati wa kuelekea sikukuu za Krismas na mwaka mpya.

Msemaji wa Mamlaka hiyo, David Mziray (Pichani)  amesema  jijini Dar es Salaam kwamba kuna taarifa kuwa kuna baadhi ya madereva na makondakta wameibua mbaya ya kupandisha nauli kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.

Alisema wamejipanga vizuri kwani wamewaandaa vijana watakaoshirikiana na Jeshi la Polisi ili kuzikamata kampuni za mabasi ambazo zitabainika kupandisha nauli kinyume cha sheria.

 Mziray alisema katika kipindi hiki wataendesha opresheni kila siku ya kukamata kampuni ambazo zitaenda kinyume na mkataba wao wa  leseni, itatozwa fani ya  sh 25000.

Sambamba na hilo, aliwatahadhalisha wamiliki wa magari hayo kuwa makini ili kuepuka kutozwa faini ambazo kwa kiasi kikubwa zinaumiza wao na wala siyo madereva na makondakta.

“Nafahamu kweli kuna baadhi ya magari hivi sasa yamekwishaanza kupandisha nauli kutokana na kuongezeka kwa abiria wanaosafiri kwenda kuungana na familia zao katika kipindi cha kusherehekea Sikukuu ya Krismas”alisema.

Mziray alisema SUMATRA haitasita kuzifutia leseni kampuni ambazo zitaonekana kuwa sugu katika kujiingiza kwenye vitendo hivyo vya kupandisha nauli kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwaibia wananchi.

Vile vile aliwaasa abiria  kutoa ushirikiano katika operesheni hiyo ya kuzikamata kampuni zinazojihusisha na upandishaji huo wa nauli, wakati mwingine wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na abiria wenyewe kuwa wagumu kuwafichua madereva na makondakta wanaofanya hivyo.

Hata hivyo,  Mziray alitoa wito kwa wananchi kupanga nasafari zao kwa utaratibu na wala siyo kurupuka kwani mara nyingi wale wanao kurupuka kwa kutaka kusafiri siku hiyo hiyo ndiyo maranyingi wanaokumbana na ubabaishaji huo katika kupata tiketi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.