- Get link
- Other Apps
Akina mama waombolezaji wakisawazisha kaburi la
marehemu Sinjembele Julius(62) aliyeuawa kwa kupigwa na mwanae Ndele
Julius(25)
Baadhi ya waombolezaji wakishuhudia mazishi ya Sinjembele yaliyofanyika Nyumbani kwake katika kitongoji cha Igawilo kata ya Swaya Mbeya
Baadhi ya waombolezaji wakishuhudia mazishi ya Sinjembele yaliyofanyika Nyumbani kwake katika kitongoji cha Igawilo kata ya Swaya Mbeya
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya firauni,
unaweza kusema hadithi kumbe nikweli ,Mkazi wa
Swaya jijini Mbeya Ndugu Ndele
Julius amemuua mama yake mzazi kwa kumpiga mateke na ngumi kisha kutoroka
pasipo julikana Novemba 25 mwaka huu.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 10 jioni
nyumbani kwa mama huyo mara baada ya kutokea kwa ugomvi kati ya mtoto wake na
kijana mwingine hali iliyopelekea mama
huyo kuingilia ndipo alipo kutwa na mauti
huo.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema
kuwa Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliokuwepo kati ya mtoto wake na
kijana mwenzake kitendo ambacho
kilipelekea mama huyo kuingilia ugomvi huo .
Amesema wakati
mama huyo akijaribu kuamulia ugomvu huo mtoto wake alicha kupigana na
mwenzake na kuanza kumshambulia mama yake kwa kumpiga ngumi na mateke
mwilini.
Amesema mama huyo alifariki muda mchache kutokana
na kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababishiwa majeraha makuibwa
yaliyopeleka kupoteza uhai wake.
Awali akizungumzia tukio hilo Mtoto wa Kwanza wa
mama huyo Ndugu Razaro Mbwiga amesema kuwa mdogo wake alikuwa na tabia ya
kugombana na mama yake marakwamara .
Hata hivyo teyari mwili huo umekwisha chukuliwa
hospitali na kuzikwa ambapo katika maziko hayo Chama cha Muungano wa kijamii
(Mujata) umewataka vijana kujiepusha na vitendo viovu kama uvutaji bangi na
pombe za kienyeji kwani ndio chanzo cha kutokea kwa vurugu nyingi.
Mjengwa.
Comments