Kampuni ya Century Insurance yakabidhi madawati Shule ya Msingi Majani ya Chai, Kipawa


Meneja wa Kitengo cha Madai wa Kampuni ya Bima ya Century  Michael Emanuel (kulia), akimkabidhi madawati 100 yenye thamani ya sh.milioni 7.5 Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Majani ya Chai,  iliyopo Kata ya Kipawa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam leo, Mary Itimay (kushoto), madawati hayo yametokana na harambee iliyofanywa mwezi juni mwaka huu na Diwani wa Kata hiyo Bonah Kaluwa kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali ambapo sh.milioni 421 zilipatikana. Wa pili kulia ni Mkuu wa Utawala wa Kampuni hiyo Colman Macha na Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa.
 

Meneja wa Kitengo cha Madai wa Kampuni ya Bima ya Century  Michael Emanuel (kushoto), akiwaelekeza wanafunzi hao jinsi ya kubandika stika za kampuni hiyo kwenye madawati hayo.

Wanafunzi wakibandika stika katika madawati hayo.
 
Wanafunzi wakiwa wamekaa kwenye madawati hayo baada ya kukabidhiwa.

Mkuu wa Utawala wa Kampuni hiyo, Colman Macha na Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa wakiwa wamekaa na wanafunzi hao baada ya kuwakabidhi madawati hayo.
Wanafunzi hao wakifurahi baada ya kupokea msaada huo. (Picha zote na Dotto Mwaibale)
 
Shule za Kipawa zapata madawati

Na Dotto Mwaibale

SHULE tano za msingi katika Kata ya Kipawa Manispaa Ilala Dar es Salaam zimenufaika kwa msaada wa madawati yalitokana na harambee iliyofanywa na Diwani wa kata hiyo, Bonah Kaluwa.
Madawati hayo yalipatikana kupitia wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia sekta ya elimu katika kata hiyo ikiwemo Kampuni ya Bima ya Century ambayo jana, ilikabidhi madawati 100 yenye thamani ya sh. milioni 7.5 kwa Shule ya Msingi Majani ya Chai.
Meneja wa Kitengo cha Madai wa kampuni hiyo, Michael Emanuel akizungumza baada ya kukabidhi madawati hayo, alisema msaada huo ni sehemu ya mpango wao katika kusaidia sekta ya elimu nchini.
"Sisi pia ni wazazi hivyo tuna kila sababu ya kuwasaidia watoto wetu ili wawe katika mazingira mazuri ya kupata elimu, ndiyo maana tumechukua jukumu hili," alisema Emanuel.
Emanuel alisema kuwa tatizo la ukosefu wa madawati ni kubwa, hivyo kila mtu anapaswa kusaidia ili wanafunzi wapate elimu sahihi na yenye ubora.
Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonah Kaluwa akizungumza katika hafla hiyo, alisema shule takriban tano za kata hiyo zimenufaika kutokana na harambee iliyofanyika Juni mwaka huu, ambapo zilipatikana sh. milioni 421.
Alisema lengo lilikuwa ni kupata madawati 1000, hata hivyo, aliwashukuru wadau waliojitokeza kwa kuchangia kwani shule hizo zimeweza kupata na visima saba vya maji ambavyo vimegharimu sh. milioni 75.
Alizitaja shule hizo kuwa ni Mogo, Karakata, Minazi Mirefu, Airwing na Majani ya Chai.
Naye Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Majani ya Chai, Mary Itimay alisema licha ya kupata madawati hayo, tatizo kubwa walilonalo ni ukosefu wa vyumba vya madarasa.
"Madawati yapo tatizo ni vyumba vya madarasa, kwani mahitaji halisi ni vyumba 33, lakini hivi sasa tuna vyumba 14 tu," alisema Itimay.
Pia alisema shule hiyo yenye wanafunzi 2,239 ina madawati 479 ambayo yamehifadhiwa kwa ajili ya kukosa vyumba vya madarasa.
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.