KILAINI ALIKANA MWANANCHI
Friday, November 16, 2012
"Kwa masikitiko makubwa nimesoma
katika gazeti la Mwananchi kwamba nimeiponda safu ya uongozi na
sekretariati ya CCM. Mimi sijaongea na gazeti lolote juu ya uongozi wa
CCM na wala sina nia au sababu ya kuuponda uongozi huo. Ni vibaya kwa
gazeti lo lote lile kutumia jina la mtu kwa kueneza maoni yake. Kama ni
waugwana natumaini watasahihisha waliyoyaandika. Nasikitika sana kwa
waliokwazwa na hilo. Askofu Kilaini
Askofu Method Kilaini
Bukoba Catholic Diocese"
Comments