Mahakama ya Rufaa yagoma kufuta rufaa ya Lema

 Wakili Edson mbogolo akizungumza na waandishi wa habari nje ya jengo la Mahakama ya Rufaa
 Aliekuwa Mbunge wa Arusha mjini, Godbles Lema akizungumza na wafuasi wake nje ya jengo la Mahakama ya Rufaa Tanzania
 Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Godbles Lema (katikati) akitoka katika Mahakama ya Rufaa huku akiandamana na wafuasi wake.Kwa hisani ya Habari Mseto Blog  

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Rufaa Tanzania, imekataa kuifuta rufaa iliyofunguliwa mahakamani hapo na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Godbles Lema kwa maelezo kuwa mapungufu yaliyopo kwenye kikaza hukumu(decree) hayawezi kusababisha mahakama hiyo iifute rufaa iliyokatwa na Lema inayopinga hukumu iliyotolewa mwaka huu na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha  ambayo ilitengua ubunge wake.

Uamuzi huo mdogo ulitolewa jana katika Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam,na kuudhuliwa na umati wa wafuasi wa Lema na ulisomwa na Naibu Msajili wa mahakama hiyo Zahara Maruma  kwaniaba ya jopo la majaji wanaosikiliza rufaa hiyo ambao wanaongozwa na Jaji Mkuu Othman Chande , Natalia Kimaro na Salum Massati.

Akisoma uamuzi huo unaotokana na pingamizi la awali lilowasilishwa na wajibu rufaa ambao ni wananchama wa cha Mapinduzi (CCM), jimbo la Arusha Mjini wanaotetewa na  Medest Akida na Alute Mughwai,    dhidi ya mwomba rufaa(Lema) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Arusha mjini  na Mwanasheria Mkuu wa Serikali anayewakilishwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali  Timon Vitalis  wakati Lema akiwasilishwa  Method Kimomogoro na Tundu Lissu ambao jana hawakuwepo mahakamani na wakili Edson Mbogoro aliwawakilisha kwaniaba yao huku Mwanasheria Mkuu akiwakilishwa na mwanasheria wa serikali, Timon Vitalis.

Jaji Chande alisema  hivi karibuni wajibu rufaa waliwasilisha pingamizi la awali ambapo waliwasilisha hoja tatu ambapo waliomba mahakama hiyo iifute alidai kuwa kikaza hukumu  kilichotumiwa na Lema kukata rufaa kilikuwa hakina mhuri wa mahakama wala haionyeshi hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha iliyotengua ubunge wa Lema ilitolewa lini, kikaza hukumu  hakikuzingatia  Kanuni za Masijala  za Mahakama Kuu ya mwaka 2005 na kwamba kikaza hukumu hicho  kilikuwa kimekosekana maneno kama ‘hukumu hii imetolewa kwa mkono wangu’ na kuomba rufaa ya Lema ifutwe.

“Jopo langu limepitia hoja za pande mbili limefikia uamuzi wa kukubaliana na hoja ya kwanza kuwa ni kweli kikaza hukumu kilichotumiwa na Lema kukata rufaa mahakama ya rufaa kilikuwa na dosari hizo ambazo ni hakikukwa na mhuri wa tarehe  na tatizo hilo halikusababishwa na Lema ni watendaji wa mahakama waliyoaanda Kikakaza hukumu hiyo;

“Kwa sababu hiyo mahakama hii imekataa ombi la wajibu rufaa lilotaka mahakama hii ifute rufaa iliyokatwa na Lema kwa sababu eti kikataa rufaa hicho kilikuwa na mapungu hayo kwasababu licha ni kweli mahakama hii inakiri kuwepo kwa mapungufu hayo, lakini mapungufu hayo hayawezi kufanya  mahakama hii iifute rufaa ya Lema.

“Na hivyo basi mahakama hii imempatia Lema muda wa siku 14 kuanzia leo awasilishe upya  rufaa  yake  ambayo atakuwa ameifanyia marekebisho  ambapo rufaa hiyo mpya itapaswa ionyeshe ina mhuri na tarehe ya kutolewa kwa hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam’alisema Jaji Chande.

Aidha Jaji Chande alisema jopo lake limetupilia mbali hoja mbili za wajibu rufaa(makada wa CCM), zilizodai kikaza hukumu hakikuzingatia Kanuni za Masijala  ya Mahakama Kuu ya mwaka 2005 na kwamba kilikosekana maneno kama ‘hukumu imetolewa kwa mkono wangu’ , kwamba hoja hizo hazina mantiki kisheria na hivyo inazitupilia mbali ”alisema Jaji Chande.

Uamuzi huu ni wa pingamizi la awali  na hausiani na rufaa iliyokatwa na Lema mahakamani hapo kwani rufaa iliyokatwa na Lema bado haijaanza kusikilizwa.

Oktoba 2 mwaka huu, pingamizi la awali lilotolewa uamuzi wake jana lilianza kusikilizwa mjini Arusha, wakili wa Lema, Kimogoro  alidai jaji Gabriel Rwakibarila wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kutoa hukumu yake Aprili mwaka huu, ambayo ilitengua ubunge wa Lema, jarada  kesi hiyo liliamishiwa  Dar es Salaam hivyo hakukuwa na muda wa kupitia hukumu na hati ya kukazia hukumu hivyo kwani walikuwa wanaletewa nyaraka hizo kutoka Dar.

 “Waheshimiwa majaji wa Mahakama ya Rufaa, wakili mwenzetu, Mughwai, ametueleza hapa aliomba mara mbili tofauti apewe tuzo hiyo ikiwa imesahihishwa lakini hakupatiwa majibu, katika mazingira hayo alitegemea sisi tungeipata vipi?” alihoji wakili huyo huku akielezea kushangazwa na hatua ya mawakili wa wajibu rufaa kutowapa nakala ya barua hizo.

Akinukuu maamuzi mbalimbali ya mahakama hiyo kuhusiana na masuala ya hati ya kukazia hukumu pamoja na kanuni mpya za uendeshaji mashauri ya Mahakama ya Rufaa ya mwaka 2009, Wakili Kimomogoro alidai  kuwa si kila kikaza hukumu  hukumu chenye upungu kina fanya rufaa iliyokatwa na mwomba rufaa kuwa batili.

Alidai  kuwa hati ya kukazia hukumu iliyotumiwa na mtejwa wake (Lema) kukata rufaa imekidhi  vigezo vyote muhimu ikiwemo kuonyesha namba ya kesi, majina na hadhi ya wadau, mambo yaliyokuwa yakidaiwa, imeainisha kilichoamuliwa na mahakama pamoja na gharama.

Aliendelea kuieleza mahakama kuwa hata jaji aliridhika nayo ndiyo maana aliamua kuisaini jambo alilosema kuwa endapo jaji aliridhika kimakosa wao kama mawakili hawawezi kumfuata na kumwambia hapa umeridhika vibaya hebu ridhika vizuri ili tukakate rufaa bali wanachofanya wao ni kuendelea na hatua inayofuata ambayo ni kukata rufaa kama walivyofanya.

Hata hivyo Kimomogoro alidai  kuwa suala la tuzo hiyo kutogongwa muhuri si suala la jaji bali ni suala la utawala kwani anayegonga muhuri mara baada ya jaji kusaini ni msajili wa mahakama.

Alidai  kuwa makosa yaliyofanyika ni ya kawaida ambayo hayaathiri kiini cha tuzo hiyo kwa kile alichoieleza mahakama kuwa tuzo haiwezi kuwa batili kutokana na mchoro au mamlaka iliyoitoa bali kinachoangaliwa ni maamuzi yaliyo ndani ya tuzo hiyo.

Aliomba mapingamizi hayo yatupwe kwa gharama za wajibu rufaa kwani kasoro zilizojitokeza zinaweza kurekebishwa wakati shauri hilo likiendelea au kila upande ubebe gharama zake kwenye usikilizwaji wa mapingamizi hayo kutokana na kuwa upande wa wajibu rufaa nao walishaandaa rufaa panda.

Kwa upande wake wakili wa serikali aliieleza mahakama hiyo kuwa anaunga mkono hoja za waleta rufaa huku akiweka wazi kuwa hati ya kukazia hukumu hutolewa kwenye mashauri ya madai ambapo alisema kuwa kazi ya kuweka muhuri si ya jaji bali ni ya masijala ya mahakama kuu.

Baada ya uamuzi huo kutolewa jana ,Lema alizungumza na wanachama wake na waandishi wa habari nje ya jengo la Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam, ambapo alianza kwa kusema ‘Peoples  huku wafuasi wake wakiitikia Power’.

Lema alisema kwanza anawashukuru wanachama wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kuja kuudhulia mahakamani hapo na kusema aliwasili jijini jana huku akiwa na wasiwasi mkubwa na uamuzi huo uliotolewa jana na mahakama ya rufaa kwani kesi  mahakama iliaribiwa vibaya na mahakama  hivyo ndiyo maana jana alikuwa akisita kuja mahakamani hapo kuupokea uamuzi huo kwasababu hivi sasa mahakama imekuwa na sifa mbaya hali inayosababishwa wananchi wengine kuona hawawezi kupata haki zao.

“Nasema hivi kesi yangu iliaribiwa vibaya na mahakama na ninamini rufaa hii niliyokata kama haitaingiliwa na mambo ya kisiasa nitashinda rufaa yangu  na nitarejea bungeni kwa kishindo’ alisema Lema na kushangiliwa na umati.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*