MAKAMU WA RAIS KUFUNGUA MAONESHO YA NYUMBA DESEMBA 7-9

  Mkurugenzi wa Tanzania Homes Expo, Zenno Ngowi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya sekta ya nyumba yaliyoandaliwa na Kampuni ya Brand Works. Kushoto ni Mratibu wa maonesho hayo, Rita Gedi na, Richard Mvula.


DAR ES SALAAM, Tanzania

MAKAMU wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal anatarajiwa kufungua maonyesho ya taarifa sahihi za sekta ya nyumba yatakayojulikana kama  Tanzania Homes Expo, yatakayofanyika Desemba 7 hadi 9 mwaka huu Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaa leo,  Mkurugenzi wa Tanzania Homes Expo, Zenno Ngowi amesema kuwa maonyesho hayo yameandaliwa na Kampuni ya Bland Works, Ngowi amesema kuwa maonyesho hayo yanalenga kukuza sekta ya nyumba nchini kwa kukuza elimu ya umma kuhusu aina mbali mbali za huduma zinazolenga sekta hiyo.

“Maonyesho haya tumekusudia kuwa jukwaa kuu la taarifa zihusuzo makazi nchini Tanzania kwani yanatoa fursa kwa taasisi muhimu kama manispaa zetu kuelezea wananchi mambo muhimu yahusuyo sekta hii kama upatikanaji  wa ardhi, vibali vya ujenzi na mengineyo” alisema Ngowi.

Ngowi alisema kuwa maonyesho hayo yatatoa fursa kwa watoa huduma za sekta hiyo kama mikopo, bima, wakandarasi, wachora ramani, makampuni ya nyumba, makampuni ya ulinzi, marembo, vifaa vya ujenzi na mengine mengi katika kupata nafasi ya kuelezea huduma wanazozitoa.

“Tunapenda kuwaalika makampuni binafsi na umma kushiriki katika maonyesho haya muhimu kwani tumekusudia kufanya maonyesho haya mara moja kila mwaka na tunaamini yataleta mafanikio katika kutatua kero za sekta hiyo” alisema Ngowi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI