Mh. Lukuvi awafariji maporoko waliojeruhiwa na majambazi Iringa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), William Lukuvi ambaye ni mbunge wa jimbo la Isimani mkoani Iringa akimfariji paroko wa parokia ya Isimani, Angelo
Burgeo (60) na msaidizi wake Herman Myalla (36) waliolazwa katika
Hospitali ya mkoa wa Iringa kwa matitabu zaidi baada ya kuvamiwa na
majambazi juzi na kuporwa fedha zaidi ya shilingi Milioni 3.8 Picha
na Francis Godwin
Na Francis Godwin,Iringa
KUFUATIA
kuvamiwa kwa makanisa matatu mkoani Iringa na kujeruhiwa kwa paroko wa
parokia ya Ismani mkoani Iringa Rais Dkt Jakaya Kikwete atoa amfariji
paroko Angelo Burgeo (60) na msaidizi wake Herman Myalla (36)
waliojeruhiwa na majambazi huku akiziomba taasisi za dini kutoa
ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuimarisha ulinzi katika maeneo
yao kama njia ya kukomesha matukio ya ujambazi yanayofanyika katika
maeneo ya taasisi za dini.
Rais Dkt
Kikwete alitoa wito huo kupitia waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera), William Lukuvi ambaye ni mbunge wa jimbo la Isimani mkoani
Iringa ambako paroko huyo na mwenzake walivamiwa ,alitoa wito huo
jana katika hospitali ya mkoa wa Iringa alipokuwa akiwasilisha salamu za
Rais Jakaya Kikwete na kutoa pole kwa Paroko Angelo Burgeo (60) na
msaidizi wake Herman Myalla (36) wa Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani,
wilayani Iringa.
Novemba 15,
mwaka huu mapadri hao ambao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa
wakiendelea na matibabu, walivamia na kushambuliwa kwa silaha za moto,
mapanga na nondo na majambazi.
Watu watano
wanaosikiliwa na polisi wakihusishwa na uhalifu huo katika tukio hilo
ambalo mapadri hao mbali na kujeruhiwa vibaya waliibiwa zaidi ya sh
Milioni 3.8.
Akiwasilisha
salamu za Rais, Lukuvi alisema ametumwa kutoa pole kwa wahanga hao,
waumini na viongozi wa dhehebu hilo la dini kwa ujumla wake.
“Tupo pamoja
nanyi katika kipindi hiki kigumu ambacho majambazi wamekuwa wakiwavamia
viongozi wa dhehebu hili la dini wakiamini mmehifadhi fedha na mali
nyingine nyingi ndani ya parokia zenu,” alisema.
Alisema tukio
la mapadri hao kuvamiwa na kujeruhiwa mkoani Iringa limekuja miezi
michache baada ya matukio kama hayo kutokea katika parokia za Migori na
Pawaga mkoani Iringa.
“Serikali
imefanya kazi ya kutoa mafunzo kwa mgambo wengi karibu katika kila
kijiji, ni wajibu wa taasisi hizi za dini kuwatumia hao au vinginevyo
ikubali kushirikiana na jeshi la Polisi kutoa mafunzo kwa walinzi wao,”
alisema.
Akipokea
salamu hizo, Padro Burgeo alisema majambazi hao walifanikiwa kuingia
ndani ya parokia yake baada ya kutumia lango la nyuma na kufanikiwa
kuwapiga chenga walinzi wao.
Alisema katika tukio hilo ilikuwa afe lakini Mungu amesaidia kuyanusuru maisha yake baada ya kufikishwa mikononi mwa madaktari.
Kaimu wa
Mganga Mkuu wa Mkoa Dk Faustine Gwanchele alisema baada ya kumfanyia
upasuaji na kutoa risasi tatu kwa Padri Burgeo hali yake inaendelea
vizuri pamoja na kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari
Comments