MICHAEL YOMBAYOMBA KUPAMBANA NA SAID OMAR 'GOGO POA' KUCHANGIA WAGOJWA WA MOYO
MABONDIA
wazamani walioiletea nchi Medali katika mashindano ya All Africa Games
na Jumuiya ya Madola miaka ya 1998, Michael Yombayomba na Said Omari
'Gogo Poa' wamejitolea kupanda ulingoni kutwangana kwa ajili ya
kuchangia watoto wenye matatizo ya Moyo.
Yombayomba,
ambaye alitwaa medali ya dhahabu katika mashindano ya Jumuia ya Madola
katika miaka hiyo ya 1998 na Gogo Poa wameamua kutwangana ikiwa ni
sehemu ya mchango wao kwa watoto hao huku wakisisitiza wadau kuunga
mkono tukio hilo.
Akizungumza
na gaazeti hili Gogo Poa alisema pambano hilo litafanyika Januari 25
mwakani ambapo pia litasindikizwa na mapambano ya mabondia mbalimbali
wenye viwango vya juu nchini.
"Tumeguswa
sana na tatizo hili la watoto wanaougua ugonjwa wa moyo ambao wengi wao
hukosa fedha kwa ajili ya matibabu hivyo sisi kama sehemu ya jamii
tutahamasisha uchagiaji wa fedha kwa kujitolea kupanda ulingoni na
chochote kitakachopatikana itakuwa ni sehemu ya mchango wetu,"alisema
Gogo Poa.
Aliwaomba
wadhamini na wadau mbalimbali kujitokeza kuzamini mchezo huo ambao una
tija ya kuchangia watoto hawo kwani ata wao walikuwa watoto ndio mana
wamekuwa katika afya nzuri na kucheza mchezo huo na kuiletea sifa taifa
hili kwa kuleta Medali
Hivyo
na watoto hawo wanatakiwa wawe na Afya njema ili wapate kuja kurithi
nyayo zetu bila afya ya mtoto michezo yote akuna kwa kuwa vipaji vingi
vinangaliwa ukiwa mtoto
Comments