MSANII KERI HILSON, KUTUA DESEMBA KUPIGA SHOO TANZANIA NA KENYA
NEW YORK, Marekani
MSANII
kutoka jijini New York, Keri Hilson, anayetamba na nyimbo zake kali
kama ‘That way you love me’, ‘Pretty girl Rock’ na ngoma nyingine,
anatarajia kutua nchini hivi karibuni kwa ajili ya kudondosha bonge la
Shoo, ambapo pia atamalizia shaoo yake nchini Kenya, Imeelezwa.
Taarifa
hizo zimetolewa na Msanii huyo katika ukurasa wake wa Mtandao wa
Kijamii wa Twitter, ambapo ameweka wazi kuwa anatarajia kuwasili nchini
mwezi ujao wa Desemba, ambapo amesema kuwa hiyo itakuwa ni mara yake ya
kwanza kufanya Shoo katika Nchi za Afrika Mashariki hususan kwa nchi
kama Tanzania na Kenya.
Comments