MTOTO ALIYEUNGUZWA MKONO NA KULISHWA KINYESI AKATWA MKONO HOSPITALI YA RUFAA YA MBEYA
Hatimaye yule mtoto aliyechomwa moto na mama yake amekatwa mkono wake wa kushoto. |
Bahati Rukangara huyu ndiye aliyemchoma mtoto Janeth. |
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Katika hali isiyo ya Kawaida Mkazi
wa majengo jijini Mbeya Ndugu Bahati Rukangara amemchoma moto mtoto mdogo wa
mika 3 aliyefahamika kwa jina la Aneth kisha kumfungia Ndani na kumlazimisha ale
kinyesi chake.
Akizungumza Mwenyekiti wa mtaa huo
Ndugu Habiba Mwakitabu amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa 10 :30
asabuhi ambapo majirani na mwanamke huyo waligundua mara baada ya kusikia sauti
ya mtoto huyo akilia kutokana na maumivu.
Amesema mara baada ya kusikia sauti
hiyo walifika eno hilo na kunza kumhoji ili kufahamu kiini cha tatizo hilo
ambapo alishindwa kutoa ushirikiano ndipo walipo anza
kumpiga.
Amesema kutokana na hali hiyo
majirani walilazimika kubomoa mlango ndipo walipo mkuta mtoto huyo akiwa uchi
huku ameungua vibaya mwilini hasa katika upande mmoja eneo la mkono wa kushoto
.
Amesema mara baada ya kumhoji mtoto
huyo aliwaeleza kuwa mama yake mdogo alichukua nguo na mkumfunga mkononi kisha
kumwagia maji ya moto pamoja na kumlazimisha ale kinyesi chake hali ambayo
iliwafanya washindwe kuvumilia na kuanza kupiga kelele kwa lengo la kuomba
msaada kwa watu wengine.
Kwa mujibu maelezo ya mwenyekiti
huyo amesema kuwa Mtuhumiwa huyo amekuwa akifanya vitendo vya manyanyaso kwa
mtoto huyo marakwamara ambapo wamekuwa wakimuonya lakini amekuwa si mtu wa
kusikia.
Ameesema mtoto huyo si wa kwa
kwake kwani amekuwa akiishi naye kwa muda mrefu sasa ambapo aliachiwa na dada
yake ambaye hakufahamika kuwa anaishi wapi kwa sasa.
Hata Diwani wa kata hiyo Ndugu
Samuel Mamboma alifika eneo hilo tukio na kutoa msaada wa usafiri kwa lengo la
kumfikisha mama huyo polisi pamoja na mtoto huyo ambaye naye alikimbizwa
Hospitali.
Hata hivyo amesema tukio hilo si la
kwanza kutokea katika meaeno hayo kwani kumekuwepo na matukio mengi hasa ya
utoaji mimba na kutupwa watoto. KWA HISANI YA MBEYA YETU BLOG
Comments