NASSIB RAMADHANI NA FRANCIS MIYAYUSHO KUGOMBANIA UBINGWA WA WBF SIKU YA UHURU WA TANGANYIKA

Mabondia Nassibu Ramadhani na Fransic Miyayusho wakitunishiana misuri wakati wa kutambulisha mpambano wao wa ubingwa wa WBF utakaofanyika Desemba 9 katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mwandaji wa mpambano wa ubingwa wa WBF Mohamed Bawazir katikati akiwa ameshika mkanda na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Fransic Miyayusho kulia wengine kulia ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa ambao na wasimamizi wa mpambano huo na Kushoto ni Mratibu Paul Kunanga na Kocha wa Nasibu Christopher Mzazi

Mabondia Nassibu Ramadhani na Fransic Miyayusho wakitunishiana misuri wakati wa kutambulisha mpambano wao wa ubingwa wa WBF utakaofanyika Desemba 9 katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Nassibu Ramadhani na Fransic Miyayusho wakitunishiana misuri wakati wa kutambulisha mpambano wao wa ubingwa wa WBF utakaofanyika Desemba 9 katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam

Na Richard Mwaikenda

MABONDIA Francis Miyeyusho na Nasib Ramadhan wana kupambana Siku ys Uhuru kwenye Ukumbi wa PTA, viwanja vya Sabasaba, Dar es Salaam, kuwania mkanda wa ubingwa wa Mabara wa Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF).

Akizunguza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Darworld Links Ltd, inayoratibu pambano hilo, Mohamed Bawazir alisema  mabondia hao mahili wataoneshana umwamba kwa raundi 12.

Alisema wapenzi wa mchezo huo watafaidika zaidi kwa kushuhudia mapambano matano makali ya utangulizi.

Aliwaja watakaotwangana katika ni utangulizi; Fadil Majia dhidi ya Juma Fundi (raundi 8), Mohamed Matumla na Doi Miyeyusho (raundi 6), Ibrahim Class dhidi ya Said Mundi (raundi 8), Fred Sayuni na Deo Samwel (raundi 6) na Hassan Kidebe dhidi ya Baina Mazola (raundi 6).

Mabondia hao walipata wasaa wa kutambiana ambapo, Ramadhan aliwaomba wapenzi wa mchezo huo kutokosa kushuhudia wakati akimwadhiri vibaya kaka yake Miyeyusho.

Miyeyusho alimuonya mdogo wake huyo, kukubali kupigana na yeye ni sawa na kudandia mbele ya treni lililoko kwenye mwendo, ambapo madhara yake ni kukanyagwa, hivyo wapenzi wa ndondi wategemee kuona jinsi atakavyomchakaza.

Pambano hilo litakalosimamiwa na Shirikisho la Masumbwi Tanzania (PST), linadhaminiwa na JB Belmont Hotel, gazeti la Jambo Leo na Kituo cha Redio cha Times Fm.

 
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA