NGASSA ATETEMESHA KAMPALA BALAA, WAGANDA TUMBO JOTO

Ngassa alivyokuwa akiteleza kushoto mwa uwanja wa namboole jana, balaa

Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
SALUTI kwa Mrisho Khalfan Ngassa. Waganda, wamekoma naye. Mashabiki wa soka Uganda, wamekoshwa na soka ya Mrisho Khalfan Ngassa wa Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge inayoendelea mjini hapa.
Wakizugumza baada ya mechi kati ya Sudan na Tanzania, mashabiki walikuwa wakimsifia mno mchezaji huyo wa Tanzania Bara aliyekuwa amevalia jezi namba nane na kusema hawajui siku Stars ikikutana na Uganda itakuwaje mbele ya mshambuliaji huyo wa Simba SC ya Dar es Salaam.
Hata Waandishi wa Habari wa Uganda, wamemsifia mno Ngassa wakisema huyo ndiye mchezaji aliyeonyesha kiwango kikubwa zaidi cha uchezaji hadi sasa kwenye michuano hii.
Ngassa jana alikuwa mwiba kweli mbele ya Sudan, akitengeneza mabao yote mawili ya ushindi yaliyofungwa na mshambuliaji John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC.
Jana Ngassa alipangwa wingi ya kushoto ambako alikuwa akiteleza kwa kasi na kutoa krosi nzuri ambazo bahati mbaya au nzuri ni mbili tu zilizotumiwa vyema na Bocco.
Mashabiki wamemsifia pia Ngassa kwamba si mchezaji mchoyo ambaye muda wote anafikiria zaidi kuwatengenezea wenzake nafasi kuliko kutaka kufunga mwenyewe.
Ngassa ni kati ya wachezaji 10 wa Simba wanaocheza michuano ya mwaka huu mjini hapa, wengine wakiwa ni Nassor Masoud 'Cholo' (Zanzibar), Juma Kaseja (Bara), Shomari Kapombe (Bara) Amir Maftah (Bara), Amri Kiemba, (Bara) Mwinyi Kazimoto (Bara), Ramadhani Singano ‘Messi’ (Bara), Christopher Edward (Bara) na Emanuel Okwi (Uganda).
Timu nyingine za Bara zenye wachezaji hapa ni Azam tisa, Mwadini Ali (Zanzibar), Abdulaghan Gulam (Zanzibar ), Samir Haji Nuhu(Zanzibar), Aggrey Morris(Zanzibar), Khamis Mcha 'Vialli'(Zanzibar), Deogratius Munishi ‘Dida’ (Bara), Erasto Nyoni (Bara), Salum Abubakar ‘Sure Boy’ (Bara) na John Bocco ‘Adebayor’ (Bara).
Yanga ina wachezaji saba, ambao ni Nadir Haroub Ali 'Canavaro'(Zanzibar), Haruna Niyonzima (Rwanda), Hamisi Kiiza (Uganda), Kevin Yondan (Bara), Athuman Iddi ‘Chuji’ (Bara), Frank Domayo (Bara) na Simon Msuva (Bara), wakati Mtibwa Sugar inao watatu Twaha Mohammed (Zanzibar), Issa Rashid (Bara) na Shaaban Nditi (Bara), JKT Oljoro ina mmoja Amir Hamad (Zanzibar) sawa na Coastal Union Suleiman Kassim 'Selembe' wa  Zanzibar pia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI