Jogoo wangu aliye kulia akipambana na jogoo wa jirani baada ya kuvamia himaya ya jogoo huyo jirani jana karibu na Kanila la Kiinjili la Kiutheri TRanzania Mtaa wa Kivule, Ukonga, Dar es Salaam. Jogoo wangu ambaye nilipanga kwenda kumtolea mungu kanisani, aliruka kutoka kwenye gari wakati namchukua kwenye buti ili niimpatie mmoja wa watoto wangu waliokuwa wakipata kimaira.
Jogoo huoyo aliruka na kuanza kukimbia. Ndipo alipokwenda kukutana na jogoo mwingine ambaye baada ya kumuona anaingilia himaya yake alikasirika na kuanza kupigana naye kwa lengo la kumfukuza eneo hilo. Mapigano hayo yaliyoshuhudiwa na baadhi ya wakazi wa eneo hilo yalidumu kwa takribani nusu saa. Baada ya hapo niliwaita vijana waliomkbiza na kufanikiwa kumkamata, ndipo nikamchukua na kwenda kumkabidhi Mwinjilisti na baadaye kunadiwa kwa sh. 45,000. Picha na Kamanda Richard Mwaikenda)
Comments