NYAMLANI ATEULIWA KAMATI YA AFCON 2013
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF),
Athuman Nyamlani ameteuliwa kuwemo kwenye ujumbe rasmi wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Afrika (CAF) utakaosimamia Fainali za Kombe la Mataifa ya
Afrika (AFCON) zitakazofanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini.
Uteuzi
huo umefanywa na Rais wa CAF, Issa Hayatou na Kamati yake ya Utendaji.
Ujumbe huo wa CAF kwa ajili ya fainali hizo zitakazoanza Januari 19 na
kumalizika Februari 10 mwaka huu una jumla ya watu 148.
Nyamlani
ni mmoja wa wajumbe watatu watakaoshughulikia masuala ya rufani.
Wajumbe wengine ni Prosper Abega kutoka Cameroon na Pierre-Alain
Monguengui wa Gabon. Nyamlani ni mjumbe wa Bodi ya Rufani ya CAF yenye
watu 12.
Comments