RIPOTI YA UNESCO YAONYESHA KUWA ELIMU BADO NI KIKWAZO KIKUBWA KWA USTAWI WA VIJANA TANZANIA NA AFRIKA
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa
nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou akizungumza wakati wa uzinduzi wa
‘Education for All Global Report’ ya mwaka 2012 inayoandaliwa na UNESCO
kila mwaka, ambapo pamoja mambo mengi aliyoyazungumzia pia amesema
tukiwa tumebakiwa na si zaidi ya miaka mitatu kufikia mwaka 2015,
michakato ya kutimiza Malengo ya Maendeleo ya Millenia (MDGs) na Malengo
ya ‘Elimu Kwa Wote’ (EFA) lazima irekebishwe.
Ameongeza kuwa japo Tanzania
inakaribia kutimiza lengo namba 2 la MDGs la ‘Elimu ya Msingi kwa Wote
na lengo la Tatu la Usawa wa Kijinsia lakini bado ziko changamoto,
akitolea mfano katika elimu na kusema msisitizo umeelekezwa katika
kuongezwa kwa idadi ya watoto wanaojiunga shule lakini kimsingi
kinachotakiwa ni kuweka mkazo kwenye kiwango cha elimu kinachotolewa.
Mwakilishi wa Shirika la UNESCO nchini
Tanzania Vibeke Jensen akiwasilisha matokeo ya ripoti ya 10 ya ya mwaka
2012 ya ‘Education for All Global leo jijini Dar es Salaam inayoitwa
“Putting Education to Work” na kufafanua kuwa takriban vijana milioni 2
nchini Tanzania hawajamaliza elimu ya msingi na hawana maarifa ya
kuwapatia kazi itakayowapatia kipato cha kujikimu kimaisha.
Amesema matokeo ya ripoti hiyo
yanaonyesha kuwa juhudi za haraka zinahitajika ili kuwekeza katika
kuwapatia vijana elimu haswa wenye miaka kati ya 15 hadi 24 Tanzania na
barani Afrika kwa ujumla.
Mwenyekiti wa Taifa Chama cha Vijana
wa Umoja wa Mataifa (YUNA) Bw. Lwidiko Edward Mhamilawa akizungumza
katika uzinduzi huo na kuitaka Serikali kuangalia upya Sera ya Elimu kwa
kuwa haimwezeshi Mhitimu kuwa na uwezo wa kufanya kazi itakayomwezesha
kuendesha maisha yake na hivyo kuwa moja ya changamoto kubwa inayoongeza
idadi ya vijana wasiona ajira mtaani.
Kamishna wa Elimu Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Profesa Eustella Bhalalusesa wakati wa uzinduzi wa
ripoti hiyo ambapo amesema Tanzania itaendelea kufanya kazi bega kwa
bega na mashirika ya Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha Sera za Elimu
zinaboreshwa ili kuinua kiwango cha Elimu na kumjenga kijana kuwa na
stadi za kukabiliana na maisha hata kama hakufaulu darasani.
Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani
nchini Tanzania (ILO) Bw. Alexio Musindo akisisitiza ili kuboresha elimu
walimu wanahitaji kupewa mafunzo bora, kupatiwa vifaa vya kufundishia
na mtaala wa Elimu kutoka ngazi ya Taifa mpaka ngazi za chini unahitaji
kufuatiliwa na kusimamiwa.
Moderator wakati wa kuchangia maoni
Juu ya Ripoti hiyo Profesa Idrissa Mshoro akitoa tathmini yake kuhusiana
na matokeo ya "Education For All Global Monitoring Report" kabla ya
kutoa nafasi kwa jopo la wataalam waliohudhuria kuendelea na uchambuzi
wao.
Jopo la Wadau wa Kimataifa wa Elimu
wakitathmini Ripoti ya UNESCO ya Mwaka 2012. Kutoka kushoto ni Moderator
Profesa Idrissa Mshoro, Deputy Head of Mission, Head of Development
Cooperation Division Ubalozi wa Sweden B. Maria Van Berlekom, TVET
Section Makao Makuu ya UNESCO Paris Bw. Borhene Chakroun, Senior
Technical Advisor, Education for Employment Bw. Peter Loan na Mjumbe wa
Bodi ya Chama cha Waajiri Tanzania Bw. Kabeho Solo.
Meneja Mipango wa Ubalozi wa Shirika
la Maendeleo la Itali katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo katika
Ubalozi wa Italia nchini Bw. Daniele Cristian Passalacqua akichangia
maoni juu wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo. Kulia ni Mwakilishi wa
Shirika la UNESCO nchini Tanzania Bi. Vibeke Jensen.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa
nchini Dkt. Alberic Kacou na Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO)
nchini Tanzania Bw. Alexio Musindo.
Pichani Juu na Chini ni Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka Mashirika ya Maendeleo, Mashirika ya Kijamii na Sekta Binafsi.
You might also like:
Comments