SWAHILI FASHION WEEK 2012 YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM
*SWAHILI FASHION WEEK 2012 YAZINDULIWA RASMI,
*KUSHEHEREKEA MIAKA MITANO
*WABUNIFU 23 KUTOKA TANZANIA KUONYESHA UBUNIFU WAO
Onyesho
kubwa la mitindo la Afrika Mashariki na kati linarajiwa kufanyika siku
tatu mfululizo katika Hoteli ya Golden Tulip kuanzia tarehe 6, 7 na 8
Desemba, 2012 ikiwa ni mara ya tano tangu kuanzishwa kwake.
Swahili
Fashion Week 2012 kwa ujumla itakutanisha pamoja wadau 50 katika tasnia
ya Mitindo kutoka nchi zinazozungumza Kiswahili na nyengine kuweza
kuonyesha ubunifu wao na kutoa mustakabali wa mwenendo wa tasnia ya
mitindo katika ukanda huu.
“Mwaka
tumekuwa kwa kiasi kikubwa, wabunifu 23 kutoka Tanzania wataweza
kuonyesha ubunifu wao na wengine waliobaki ni kutoka nje ya Tanzania,
ambao wote wataonyesha ubunifu wao katika jukwaa moja ukiachilia
wabunifu 16 walionyesha ubunifu wao katika maonyesha ya Swahili Fashion
Week yaliyofanyika Nairobi, Kenya, Oktoba 6, 2012” Alisema Meneja wa
Swahili Fashion Week, Washington Benbella
Katika
kuongeza maonyesho ya mitindo, mwaka huu Swahili Fashion Week shopping
Festival ambayo ilianza 2010 itakuwepo tena kwa mara nyengine ambapo
itashirikisha zaidi ya waonyeshaji 30 katika sehemu moja ikiwa ni kwa
ajili ya kuonyesha na kuuza bidhaa za ubunifu hivyo kuifanya kuwa msimu
mkubwa manunuzi ya kazi za ubunifu wa mitindo hapa Tanzania.
Kama
ilivyo ada, Swahili Fashion Week inatoa nafasi kwa kuendeleza vipaji,
ambapo tarehe 24 Novemba, 2012 kutakuwa na mchujo wa wazi kwa
wanamitindo wapya na wanaochipukia kwa jinsia zote, na mnamo tarehe 7
Desemba, 2012 kutakuwa na warsha kwa ajili ya wabunifu wote Tanzania
chini wadhamini wakuu wa warsha hiyo USAID Compete ambayo itafanyika
katika Hotel ya Golden Tulip” Aliongeza Benbella
Mashindano
tofauti yamepangwa kufanyika wakati wa Swahili Fashion Week, ikiwemo
Shindano la kumtafuta Mbunifu Bora anaechipukia na Mbunifu Bora wa
kubuni Fulana. Sio tu inatoa changamoto na ari ya ushindani katika
tasnia ya ubunifu nchini Tanzania, bali pia inaweka msingi imara kwa
wabunifu wa baadae.
“Sherehe
maalum za kufungua Swahili Fashion Week zinarajiwa kufanyika siku ya
Jumapili tarehe 25 Novemba, 2012, Thai Village kuanzia saa 9 usiku.
Sherehe hizo pia zitafuatiwa na kutangazwa kwa majina ya waliochaguliwa
kushindania tuzo mbalimbali zilizowekwa katika vipengele 16, tuzo hizi
ni za kwanza na ndio pekee katika ukanda huu. Tiketi za sherehe za
uzinduzi wa Swahili Fashion Week 2012 zinapatikana sehemu zifuatazo,
Thai Vilage, Mgahawa wa Epidor uliopo Masaki, na Tanzania Mitindo House”
Alisema Meneja Uhusiano, Hassan Mrope
“Tukiwa
na mipango yenye ndoto za kutangaza biashara ya mitindo katika ukanda
wa Afrika mashariki na kati, ninapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru
washirika wetu pamoja na wadhamini
wetu ambao karibia ya wote wamekuwa wakitusaidia kutokea maonyesha
yaliyopita mpaka sasa. Pia tuwashukuru sana watu wote wanaosaidia tasnia
ya mitindo hapa Tanzania kwa si tu kuhudhuria matamasha na maonyesho
kama haya bali pia kwa kununua bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini kwani
hii inatangaza kinachotengenezwa Africa “Made in Africa”. Alimalizia
Benbella
Swahili
Fashion Week 2012 imedhaminiwa na Vodacom, USAID Compete, Origin
Africa, EATV, East Africa Radio, Golden Tulip Hotel. Amarula, Precision
Air, 2M Media, Global Outdoor Ltd, Vayle Springs Ltd, Eventlites,
Ultimate Security, BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania), Perfect Machinery Ltd, Ndibstyles, PKF Tanzania and 361 Degrees.
KUHUSU SWAHILI FASHION WEEK
Swahili Fashion Week ni jukwaa kubwa la mitindo ya mavazi la kila mwaka katika ukanda wa Afrika mashariki na kati kwa sasa. Huu ni mwaka wa Tano sasa,
ambapo Swahili Fashion Week imekuwa ni Jukwaa la wanamitindo na
watengeneza vito vya urembo kutoka katika nchi zinazoongea Kiswahili na
bara zima la Afrika kwa ujumla kuweza kuonesha vipaji, kutangaza ubunifu
wao na kukuza mtandao wa mawasiliano ya kibiashara ndani na nje ya nchi
kwa wadau wa mitindo. Hili limelenga kuhamasisha ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati kwamba ubunifu wa mavazi ni njia moja wapo ya kujipatia kipato na wakati huo huo kukuza bidhaa zinazotengenezwa Afrika ( Made in Africa concept)
Ikiwa
imeanzisha uhai na jukwaa la matumaini kwa kilinge cha mitindo katika
ukanda huu, Swahili Fashion Week Swahili Fashion week imelenga kuwa
maonyesho ya ubunifu wa mavazi linaloonekana sana Afrika na hasa kwa
ajili ya soko la kimataifa, lililoundwa, kutengenezwa na kujengwa mwaka
2008 na Mustafa Hassanali.
Ifikapo
mwaka 2013, Swahili Fashion Week ina lengo la kuwa ni tukio
litakalotokea mara mbili kwa mwaka, ambapo kwa kuanza tukio la kwanza
litafanyika nchini Kenya kama sehemu ya kwanza kisha tukio lenyewe
kabisa kufanyika baadae nchini Tanzania kama sehemu
Comments