TAIFA STARS YAINYUKA HARAMBEE STARS 1-0 CCM KIRUMBA
TIMU
ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo imeibuka na ushindi wa bao 1-0
dhidi ya Harambee Stars, ya Kenya katika mchezo wa kirafiki wa Kimataifa
uliomalizika hivi punde katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Bao
la Stars, limefungwa mapema tu katika dakika ya 5 na sekunde kadhaa
kipindi cha kwanza na Agrey Moris, na kufanya timu hizo zikienda
mapumziko Stars ikiwa mbele matokeo yaliyodumu hadi kumalizika kwa
mchezo huo.
Comments