TRA YAZIFUNGA AKAUNTI ZA TFF, MZUNGUKO WA PILI VPL HATIHATI
Sunday Kayuni, Mkurugenzi wa Ufundi, TFF
MZUNGUKO
wa pili wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara huko mashakani kufanyika
baada ya Mapato ya Taifa(TRA) kuzifunga akaunti za udhamini wa ligi
hiyo.
TRA
ilizifunga akaunti za TFF ikiwemo ya udhamini wa ligi hiyo ikiwa ni
sehemu ya kulishinikiza Shirikisho la Soka nchini(TFF) kulipa makato ya
kodi kwenye mishahara ya timu ya taifa(Taifa Stars) tokea kipindi cha
kocha Marcio Maximo.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka
nchini(TFF) Sunday Kayuni alisema mishahara ya makocha wa Taifa Stars
tangia kocha Marcio Maximo ilikuwa haikatwi kodi na hivyo kufanya
gharama wanazodaiwa na mamlaka ya Mapato kufikia shilingi milioni
157,407.968.00.
Alisema
wamekuwa wakipata taarifa ya mara kwa mara toka TRA ikiwakumbusha juu
ya makato hao na wao kuwajibu kuwa hawahusiki kwenye malipo ya mishahara
ya makocha hao kwani ni waajiriwa wa Serikali.
Kayuni
alisema hata hivyo kwa kuwa wao ndio walezi wa makocha hao TRA imeamua
kuzifunga akaunti zao ikiwemo ya udhamini wa Ligi Kuu ya Soka ya
Tanzania Bara ambayo ina zaidi ya shilingi milioni 300.
Alisema
kutokana na hali hiyo walifanya mazungumzo ya mara kwa mara na TRA bila
ya mafanikio na kuamua kuunda kamati itayoshirikisha Kamati ya Ligi
ikishirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kwa
ajili ya kufanya mazungumzo na mamlaka hiyo ya mapato nchini.
“Tunaona
labda tukiunganisha nguvu zetu labda wenzetu wa TRA wanaweza
kutusikiliza, hivyo Kamati tutakayounda kwa kushirikiana na wizara
itakwenda kujaribu kufanya tena mazungumzo na TRA.”alisema Kayuni.
Kwenye
Mkutano huo na waandishi wa habari Kayuni aliambatana na Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi Kuu Saidi Mohamedi na Mkurugenzi Mkuu wa
Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara Silas Mwakibinga, ambao wote
walionyesha umuhimu wa kuunganisha nguvu zao kuishawishi TRA.
Comments