Wananchi Tabata Kimanga watoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya

 
Askari Polisi akiwatuliza wanafunzi  wa Shule ya Msingi Tabata Kimanga, Dar es Salaam, waliofika kuwasikiliza wananchi waliokuwa wakitoa maoni yao mbele ya wajumbe wa  Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyofika maeneo hayo leo.
 
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Magoza Tabata, wakijaza fomu kwa ajili ya kutoa maoni yao, mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, waliofika maeneo ya Tabata Kimanga, Dar es Salaam jana, kusikiliza maoni ya wananchi leo.

 
Baadhi ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, wakisikiliza maoni ya wakazi wa Tabata Kimanga, Dar es Salaam, wakati wajumbe hao walipofika maeneo hayo leo kuchukua maoni ya wananchi.


 Mwananchi wa Tabata Kimanga, Makame Mpate, akitoa maoni yake mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyofika maeneo hayo jana kuchukua maoni ya wananchi.

 Wananchi waliofika kwenye mkutano wa kukusanya maoni ya Katiba mpya, wakisikiliza maoni yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya wananchi, mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwenye mkutano huo.
Mwananchi wa Tabata Kimanga, Dar es Salaam, Mchungaji Gordon Kangaulaya, akitoa maoni yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Katiba, iliyofika maeneo hayo leo kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI