Wananchi Tabata Kimanga watoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya
Askari Polisi akiwatuliza wanafunzi wa Shule ya Msingi Tabata Kimanga, Dar es
Salaam, waliofika kuwasikiliza wananchi waliokuwa wakitoa maoni yao mbele ya
wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,
iliyofika maeneo hayo leo.
Baadhi ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko
ya Katiba, wakisikiliza maoni ya wakazi wa Tabata Kimanga, Dar es Salaam,
wakati wajumbe hao walipofika maeneo hayo leo kuchukua maoni ya wananchi.
Mwananchi wa Tabata Kimanga, Makame Mpate, akitoa maoni yake mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyofika maeneo hayo jana kuchukua maoni ya wananchi.
Wananchi waliofika kwenye mkutano wa kukusanya maoni ya Katiba mpya, wakisikiliza maoni yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya wananchi, mbele ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwenye mkutano huo.
Comments