WAREMBO MISS EAST AFRICA KUANZA KUWASILI KESHO
Warembo
wanaoshiriki mashindano ya Miss East Africa 2012 wanatarajiwa kuanza
kuwasili kesho jijini Dar es salaam wakitokea katika Nchi mbalimbali
tayari kwa mashindano hayo makubwa yatakayo fanyika tarehe 07 December
katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam
wakati huo huo Mtangazaji mashuhuri wa Mnet na ambae amewahi kuwa
mshindi wa Big Brother Africa, Gaetano Kagwa anayeishi Afrika Kusini
ndiye atakaekuwa MC wa mashindano ya mwaka huu ya Miss East Africa 2012
yatakayofanyika jijini dar es salaam
Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitashirikisha warembo
kutoka Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia,
Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion,
Comoros, Seychelles, na Mauritius na warembo mbalimbali wa Afrika
mashariki walioshindana katika Nchi mbalimbali za Ulaya
Mashindano ya Mwaka huu yanayosubiliwa kwa hamu yanatarajiwa
kushuhudiwa na mamilioni ya watu Duniani kupitia kwenye luninga zao na
pia kwa njia ya Internet ambapo yatautangaza utalii wa Tanzania kwa
kiasi kikubwa na pia kujenga umoja wa Afrika mashariki na kudumisha
utamaduni wa ukanda huu wa Afrika.
Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam
Comments