WAREMBO WATAKAOZIWAKILISHA NCHI ZA RWANDA NA KENYA KATIKA MASHINDANO YA MISS EAST AFRIKA 2012
Mwakilishi wa Kenya katika shindano la
Miss East Africa 2012.
...
Mrembo atakae iwakilisha Rwanda ni
UMWARI NEEMA (22) ambae ana urefu wa futi 5.9 ambae ni mwanafunzi wa mwaka wa
tatu katika chuo cha Kigali Institue of Education ( KIE) na pia ni mfanyakazi wa
Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo jijini Kigali.
Mrembo atakaeiwakilisha Nchi ya Kenya
ni JOAN WAMBUI NDICHO (18) mwenye urefu wa futi 5.8 na anayetarajia kujiunga na
Chuo kikuu cha Machakos University College kusomea mambo ya
utalii
Fainali za mashindano ya Miss East
Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi December mwaka huu katika ukumbi wa
Mlimani City jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya,
Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi,
Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.
Mashindano ya Mwaka huu yanayosubiliwa
kwa hamu yanatarajiwa kushuhudiwa na mamilioni ya watu Duniani kupitia kwenye
luninga zao na pia kwa njia ya Internet ambapo yatautangaza utalii wa Tanzania
kwa kiasi kikubwa na pia kujenga umoja wa Afrika mashariki na kudumisha
utamaduni wa ukanda huu wa Afrika.
Mashindano ya Miss East Africa
yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es
salaam
Comments