WAWILI WAKUTWA NA SILAHA AKIWEMO MWANAMKE- MBARALI.


 Hawa Mathias wa Mbeya Yetu Blog
Jeshi la polisi Mkoani Mbeya linawashikiliwa watu wawili akiwemo mwanamke  wakazi wa kijiji cha Madibila  na Mkunywa Wilayani mbarali kwa tuhuma za kupatika na silaha pamoja na nyara za serikali  kinyume cha sheria.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari  na  kamanda wa polisi Mkoani Mbeya Athuman Diwani alisema kuwa watuhumiwa hao walikamtwa kwa nyakati tofauti  na askari wa wanayamapori (TANAPA) na akari wa jeshi la polisi walipokuwa katika doria za kusaka waharifu

Alisema kuwa katika tukio la kwanza  Christian Mhangole (40) mkulima alikamatwa na polisi akiwa na  siraha aina ya SMG   yenye namba 88560 ikiwa na risasi 50 ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika mfuko maarufu kama( sulphet  ).

Diwani alisema kuwa mara baada ya uchunguzi zaidi mtuhumiwa huyo alibainika kuwa na nyara za serikali ikiwa ni pamoja na nyama ya nyati kilo 15 ,nyama ya tembo kili 17 ambazo zilikuwa zimefichwa nyumbani kwa mtuhumiwa huyo na kwamba siraha aliyokamatwa nayo imekuwa ikimilikiwa kinyume cha sheria.

Aidha kamanda Diwani alisema mtuhumiwa baada ya kuhojiwa alikiri kujihusisha na biashara ya uwindaji haramu wa wanyama pori na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya upelelezi kukamiliki kujibu tuhuma zinazomkabili.

Katika tukio la pili mwanamke  kijiji cha Mkunywa  wilayani mbarali  Emaliana Ndemo (30) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kupatikana na siraha aina ya Reffle yenye namba B 58221 ikiwa imefichwa  chumbani ndani ya nyumba yake .

Diwani alifafanua kuwa kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kulitokana na ushirikiano mzuri baina ya wananchi na jeshi la polisi na kwamba ilikuwa ikitumiwa na mume wa mtuhumiwa aliyejulikana kwa jina za moses  mlingamolo (30) ambaye alifanikiwa kukimbia na  polisi wanaendelea na msako ili aweze kufikishwa mikononi mwa vyombo vya sheria.

Aidha kamanda wa polisi ametoa wito kwa wananchi kuwafichua watu wanaomiliki siraha kinyume cha sheria kwani wanachangia uvunjifu wa amani kwa wananchi wasiokuwa na hatia na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA