YANGA YAONGOZA LIGI, SIMBA YASHANGAA BWAWA LA MINDU

 Wachezaji wa Yanga pamoja na Azam wakiingia Uwanjani. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
  Benchi la Ufundi la timu ya Azam
 Benchi la ufundi la timu ya Yanga
 Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu akiipangua ngome ya Azam kabla ya kuachia kiki kali na kuipatia timu yake bao la kwanza.
 Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva (kushoto) akichuana na beki wa Azam, FC, Said Morad katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0.
 Wachezaji wa Yanga wakishangilia
 Mshambuliaji wa Yanga Hamisi Kiiza akiwaongoza wachezaji waenzake kushangilia bao la kwanza la lililofungwa na Didier Kavumbagu (kushoto) wakati wa mchezo wa Ligu Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0.
 Golikipa wa Azam, Ally Mwadini akiokoa moja ya hatari zilizoelekezwa langoni mwake wakati wa mchezo wao dhidi ya Yanga.
 Kikosi cha Yanga
 Kikosi cha Azam
Raha ya ushindi, hureeeeeeeeeeee
Balozi wa Fifa, Abeid Pele (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya viongozi wa TFF pamoja na Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto wakati alipohudhuria mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara kati ya Yanga na Azam FC kwenye uliuofanyika leo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Pele yupo nchini kwa  ajili ya programu za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA). 

MOROGORO, Tanzania
Kutoka mjini Morogoro Simba ya jijini Dar es Salaam leo imejikuta ikiangukia pua baada ya kuchapwa bao 2-0 na Mtibwa Sugar, mchezo litawaliwa na rabsha za mara kwa mara kutoka kwa mashabiki wa Simba waliokuwa na hasira wakidai mwamuzi Judith Gamba, alikuwa hawatendei haki.
Mtibwa ilijipatia bao dakika ya 34, kwa bao lililofungwa na Mohamed Mkopi baada ya Kipa Juma Kaseja kutema shuti kali la Vicent Barnabas.

Dakika ya 87, mshambuliaji mahiri Hussein Javu, aliipatia Mtibwa bao la pili, baada ya Kaseja kufanya mbwembwe langoni mwake.

Baada ya mchezo kumalizika, Kaseja aliangua kilio uwanjani huku mashabiki wakimzonga.
Wachezaji wa Simba waligoma kupanda basi lao, ambako baadhi ya viongozi wao walifanya kazi ya ziada kuwabembeleza, ambako walikubali kwa shingo upande, lakini baada ya muda Mrisho Ngasa alishuka akiwa kabadilisha nguo kuondoka kivyake huku akisindikizwa na mashabiki lukuki.

 Kwa matokeo ya mechii za leo, Yanga imekamata usukani rasmi ikiwa na pointi 26 huku Simba ikibaki na pointi zake 23 wote wakiwa na michezo 12 huku Azam ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi 21 huku Mtibwa ikifikisha pointi 13. 

Yanga iliwakilishwa na

Ally Mustafa Barthez, Mbuyi Twite, Oscar Joshua, Naroub Cannavaro, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima.


Azam: Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Ibrahim Shikanda, Aggrey Morris, Said Morad, Kipre Balou, Salum Abubakar, Jabir Aziz, John Boko, Kipre Tchetche, Hamis Mcha ‘Viali’.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*