Sheria ya kusimamia vyombo vya habari

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO


  
      





IDARA YA HABARI (MAELEZO)

S.L.P.  9142, Dar es Salaam, Simu:  2110585, 2122771/3, Fax: 2113814, e-mail: maelezopress@yahoo.com

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kwamba mchakato wa maandalizi ya kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari (Media Services Bill) upo katika ngazi za juu  Serikalini.

Mswada huo unatarajiwa  kuwasilishwa  Bungeni wakati wowote baada ya kupitishwa katika ngazi za juu za Serikali.

Mswada unaotarajiwa kuwasilishwa ni ahadi ya Serikali tangu mwaka 2007.  Serikali ipo tayari kupokea hoja mbalimbali baada ya kuwasilisha mswada huu Bungeni kwa maana ya kuboresha ikiwemo Haki ya Kupata Habari.

Serikali inawataka wadau wa habari na watanzania kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuhakikisha kwamba Mswada wa Kusimamia vyombo vya Habari unakamilika na kuwa sheria lengo likiwa ni kujenga misingi ya demokrasia na utawala bora.
24/1/2013

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*