BLOG YA KAMANDA WA MATUKIO YAPATA TUZO KATIKA KONGAMANO LA NHIF

Mmiliki wa Blog ya Kamanda wa Matukio, Richard Mwaikenda akionesha tuzo ya cheti aliyopatiwa na Uongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kwa kutambua mchango wake katika masuala ya mfuko huo, wakati wa Kongamano la NHIF na Wanahabari la kujadili tafiti zilizofanywa na wanahabari katika halmashauri 26 nchini kuhusu matumizi ya fedha zinazochangwa na wananchi kwa ajili ya Afya. Kongamano hilo lililoshirikisha wanahabari 150  lilimalizika mwishoni mwa wiki Mjini Mtwara.
Mkuu wa Wilaya ya Kalmbo, Moshi Chang'a (katikati) akimkabidhi tuzo hiyo Mmiliki wa Blog ya Kamanda wa Matukio, Kamanda Richard Mwaikenda. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba.
Mmiliki wa Blog ya Kamanda wa Matukio, Kamanda Richard Mwaikenda (katikati), akiwa na wanahabari wenzie wakati wa Kongamano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Benjamini Mkapa katika Chuo cya Ualimu Mtwara, mwishoni mwa wiki. Kutoka kushoto ni; Mhariri Mtendaji wa gazeti la Jamhuri, Deodatus Balile, Mtangazaji wa Televisheni ya ITV Mara, George Marato, Mtangazaji wa ITV, Dar es Salaam, Godfrey Monyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI