BREAKING NEWSS: PADRE EVARIST MUSHI WA KANISA LA MTONI ZANZIBAR AUAWA WA KUPIGWA RISASI
Hali si shwari nchini baada ya Padri
Mushi ambaye alikuwa ni Paroko wa Parokia ya Minara Miwili – Zanzibar
kuuwawa kinyama kwa kupigwa risasi .
Padri huyo ameuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana leo mida ya saa moja asubuhi akielekea kanisani
Taarifa zilizopatikana sasa hivi ni kuwa Paroko wa Kanisa la Katoliki
Minara Miwili Zanzibar, Evarist Mushi amefariki dunia baada ya kupigwa
risasi saa 1.00 asubuhi na kufariki kabla hajafika hospitali ya Mnazi
Mmoja. Paroko huyu amepigwa risasi akishuka katika gari lake wakati
akienda kuendesha ibada ya saa 3.00 leo.
Padri Evarist Mushi amepigwa risasi kichwani na kufa papohapo na watu
wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika Kanisa la
Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar.
Msemaji wa Polisi Zanzibar, Inspekta Mohamed Mhina amethibitisha tokeo hilo.
Comments