DROGBA APATA MAPOKEZI MAKUBWA UTURUKI WALIPOKUWA YANGA
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ivory Coast, Didier Drogba
amepata mapokezi mazuri alipowasili Istanbul alipokubali kujiunga na Galatasaray
ya Uturki katika uhamisho wa Januari.
Kiungo wa zamani wa Inter Milan, Wesley Sneijder
alipata mapokezi kama hayo alipowasili Uturuki mwezi uliopita na Drogba ameamua
kumfuata Mholanzi huyo akiondoka Shanghai Shenhua ya China.
Nahodha huyo wa Ivory Coast alichelewa kuwasili kwenye
timu hiyo kwa sababu ya Fainali za Mataifa ya Afrika.
Didier Drogba akiwa amezungukwa na wapiga picha baada ya
kuwasili Istanbul
Didier Drogba akiwa ameshika bendera ya Galatasaray baada
ya kuwasili Istanbul mchana wa leo
Drogba akiwa ameshika scarf yenye jina
lake
Polisi walilazimika kufanya kazi ya ziada kuwadhibiti
mashabiki waliopagawa na Drogba
Drogba alipata mapokezi sawa na aliyopata Wesley Sneijder
alipowasili Uturuki mwezi uliopita
Frenzy: Galatasaray fans hold
up a flag in tribute for the striker after his arrival at Ataturk
Airport
'Nina furaha sana kuwa hapa, kwangu ni changamoto mpya,
sehemu mpya katika maisha yangu. Nitafanya mazuri ili kupata mafanikio katika
klabu hii.'
Drogba ataungana na Emmanuel Eboue, ambaye alijiunga na
klabu hiyo bingwa ya Uturuki akitokea Arsenal mwaka 2011.
Mshambuliaji mwingine wa zamani wa Chelsea, ambaye
alitoka Stamford Bridge kwenda China, Nicolas Anelka amerejea
Ulaya.
Nicolas Anelka alijiunga na Shenhua Januari mwaka jana,
lakini ameamua kujiunga na vigogo wa Italia, Juventus, akikamilisha uhamisho
wake kwa mabingwa hao wa Serie A mwezi uliopita.
Wesley Sneijder naye alipata mapokezi
makubwa
mashabiki waliojitokeza kumpokea kiungo huyo kutoka Inter
Milan
Wesley Sneijder tayari amekwishaanza kazi
Galatasaray
Comments