KAMATI YASITISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA TFF NA TANZANIA PREMIER (TPL) BOARD
1.
Kamati ya Uchafguzi ya TFF imepitia mchakato mzima wa uchaguzi wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Uchaguzi wa Tanzania
Premier League Board (TPL Board) ili kujiridhisha kuwa mchakato mzima wa
uchaguzi unakidhi kikamilifu matakwa ya Kanuni za Uchaguzì na Katiba
ya TTF.
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF imebaini kuwa kuna matatizo ya kikanuni ambayo
yanapaswa kuzingatiwa kwanza kabla ya kuendelea na mchakato wa uchaguzi.
2.
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kwa mamlaka
iliyonayo kwa mujibu wa Ibara ya 10(5) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF
INASITISHA zoezi la uchaguzi wa Tanzania Premier League Board (TPL
Board) na Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hadi
hapo matatizo hayo ya kikanuni yatakapopata utatuzi.
3. Kamati ya Uchaguzi itawatangazia baadaye tarehe mpya za uchaguzi wa
Tanzania Premier League Board (TPL Board) na Shirikisho la Mpira we Miguu Tanzania (TFF).
Deogratias Lyatto
MWENYEKITI
KAMATI YA UCHAGUZI TFF
Comments