MAONESHO YA SHANGAA-ART OF TANZANIA YATIA FORA JIJINI NEW YORK
Queense Community Collage ambacho ni sehemu ya mtandao wa Vyuo vikuu vya
Jiji la New York ( City University of New York ) mwishoni wa wiki
kiliandaa maonesho sanaa za kitanzania. Maonesho hayo
yaliyofanyika katika Chuo hicho yanaelezwa na waandaji ni ya kwanza
kufanyika nje ya Tanzania na Ujerumani, yalipewa jina la
SHANGAA-Art of Tanzania likihusisha mkusanyiko sanaa zaidi ya 112
lakini kila moja ikibeba maudhui yake. Kwa kweli kama lilivyo jina la
maonesho hayo, ziliwashagaza wageni mbalimbali waliohudhuria maonesho
hayo. Tuvako Manongi, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa
(pichani akifungua maonyesho hayo), ndiye aliyepamba maonesho hayo kama
mgeni wa heshima, akiambatana na Mkuu wa Utawala wa Ubalozi wa
Tanzania Nchi Marekani, Bi. Lily Munanka. Sanaa zilizopamba maonyesho
hayo zilikuwa ni za kuchonga nyingi kati yake zikitoka katika Mikoa ya
Usukumani na Umakondeni. Laini pia kulikuwa na video zilizokuwa
zikionyesha aina mbalimbali za ngoma zikionyesha mila na utamaduni wa
mtanzania katika uhalisia wake. Jumla ya sanaa 121 zilikusanywa kutoka
wa wadau mbalimbali lakini ni 112 tu zilizoweza kuoneshwa kutokana na
uhaba wa nafasi. Kwa kutambua umuhimu wa maonyesho hayo Halmashauri ya
Jiji la New York ilitoa Hati kwa waandaaji wa maonesho hayo.
Comments