MJUE MGOMEA URAIS KIJANA KENYA

Peter Kenneth

Peter Kenneth(kushoto) ndiye mgombea wa urais mwenye umri mdogo kuliko wote
Peter Kenneth alizaliwa tarehe 27 Novemba mwaka 1965 na anatoka mkoa wa kati. Ndiye mgombea wa kwanza asiye na jina asilia la kiafrika.
Akiwa ndiye mgombea mwenye umri mdogo sana, anasisitiza kuwa , yeye kama kiongozi mwenye mchanganyiko wa makabila, atahakikisha kuwa ukabila ambalo ni tatizo sugu Kenya , unamalizika.
Akiwa mdogo wa umri ikilinganishwa na wagombea wengine, Kenneth mwenye umri wa miaka 47, alipigiwa debe sana kwa namna alivyoleta maendeeo katika eneo bunge lake.
Kama naibu waziri, katika serikali ya Rais Kibaki,Kenneth anagombea urais kwa muungano wa EAGLE, ambao umewaleta pamoja waliokuwa wanafunzi wenza katika shule ya sekondari ya Starehe . Mgombea mwenza wa Peter Kenneth ni meneja mkuu katika kampuni ya huduma za simu ya Safaricom.
Kenneth alikuwa mgombea wa kwanza wa urais kuzindua ruwaza yake ambayo ilitaja sekta 13 ambazo atazipatia kipaombele ikiwa atashinda urais.
Ni pamoja na kuhakikisha uwepo wa chakula, kushughulikia swala la ukosefu wa ajira, kuimarisha huduma za afya, elimu, utalii , kilimo, maji , kudhughulikia maswala ya wakenya wanaoishi ughaibuni, viwanda na uzalishaji wa bidhaa.
Anasema kuwa ananuia kuongeza uzalishaji wa chakula, kwa kutengeza miradi kumi ya unyunyiziaji maji mashamba. Pia anaahidi kuwa serikali yake itapunguza bei ya mazoa ya kilimo pamoja na kuondoa kodi ka mazao ya shambani.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI