MJUE RAILA ODINGA MGOMBEA URAIS KENYA

Raila Amolo Odinga


Raila Odinga alizaliwa Januari tarehe 7 mwaka 1945 Magharibi mwa Kenya mkoa wa Nyaza. Raila, anayejulikana kwa wafuasi wake kama "Agwambo" kumaanisha mwenyekiti kwa lugha yake asili ya Dholuo, ni waziri mkuu wa kwanza wa Kenya , wadhifa ulioundwa kufuatia mkataba wa kitaifa ulioafikiwa baada ya ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007-2008 kama ishara ya kugawana mamlaka.
Alitia saini mkataba wa kugawana mamlaka na Rais Mwai Kibaki ili kumaliza ghasia za miezi miwili zilizokumba nchi baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata.
Raila mwenye umri wa miaka 68 wa chama cha ODM ingawa kwa sasa anagombea urais kwa muungano wa CORD, ameamua kushirikiana na makamu wa Rais Kalonzo Musyoka, ambaye pia alikuwa hasimu wake miezi miwili tu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2007.
Aliondoka kutoka chama cha ODM na kuunda chama chake ODM-Kenya na hata kuitikia uteuzi wake kama makamu wa rais wa serikali ya Rais Mwai Kibaki.
Kama hayati babake, Jaramogi Oginga Odinga, Raila ambaye ni waziri mkuu wa kwanza wa Kenya, kwa miaka minane aliishi kukamatwa na kuachiliwa mara kwa mara tangu mwaka 1982 hadi 1991 kwa harakati zake za kupigania mageuzi wakati wa muhula wa pili wa utawala wa rais Daniel arap Moi.
Kufuatia kuundwa kwa katiba mpya, mwezi Agosti, mwaka 2010, amekuwa akisema kwenye kampeini zake kuwa nia yake ni kuleta mageuzi ya kisiasa.
Raila ni mwanasiasa anayesifika sana kwa ushawishi wake kisiasa na ambaye amekuwa katika msitari wa mbele kuunda vyama vya miungano na wanasiasa ambao ni mahasimu wake.
Baada ya uchaguzi wa mwaka 1997 ambapo Raila alishikilia nafasi ya tatu, kufuatia kuundwa kwa muungano wa chama chake (NDP) na chama cha rais wa zamani Daniel moi (KANU), aliteuliwa kama waziri wa kawi katika serikali ya muhula wa mwisho wa Moi.
Mwaka 2002, baada ya Moi kumuunga mkono uhuru Kenyatta, kama mrithi wake, Raila na maafisa wengine wa KANU ikiwemo Kalonzo Musyoka na wafuasi wengine, walipinga ungwaji mkono wa Kenyatta kugombea Urais. Waliungana na kiongozi wa upinzani Mwai Kibakina na kuunda muungano wa National Rainbow Coalition (Narc) ambao baadaye ulishinda uchaguzi wa mwaka 2002.
Raila aliungana na Rais Mwai Kibaki kuunda serikali ya Muungano ya NARC baada ya kumuondoa mamlakani rais mstaafu Daniel Moi
Mwaka 2005 aliungana na Uhuru Kenyatta aliyekuwa kama kiongozi rasmi wa upinzani, ili kushinda kura ya maoni kuhusu rasimu ya katiba chini ya serikali ya rais kibaki .
Wakati Kibaki alipomfuta kazi na washirika wake, aliunda chama cha ODM ambacho kilipiga kura ya La dhidi ya rasimu ya katiba mpya. Aliongoza kampeini mwaka 2007 na kwa shingo upande kukubali ushindi wa rais Kibaki
Katika uchaguzi uliokumbwa na utata , ghasia na mauaji. Lakini hatimaye alilazimika kujiunga na Kibaki katika serikali ya Muungano.
Disemba mwaka 2012, Raila alilazimika kupiga moyo konde na kurudiana na Kalonzo Musyoka chini ya muungano wa CORD, kwani daima husema katika siasa, hakuna maadui wa kudumu.
Raila anaamini kuwa wakenya wanastahili kuhudumiwa vyema zaidi kuliko ahadi wanazopewa na kwamba chini ya utawala wake, Raila anaahidi kuleta mageuzi na kuhakikisha uongozi bora. Anaahidi kuwa serikali yake itaekeza katika viwanda vya kisasa , mabohari pamoja na vituo vya teknolojia ya mawasiliano katika maeneo ya kuvulia, ushirikiano na sekta ya kibinafsi ili kuimarisha kilimo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI