Mtumishi wa Mungu ashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kutokana na kutoa lugha ya kichochezi.

picha na mbeya yetu

Muinjilisti Nicholaus Luwoneko Kamwagila mwenye umri miaka 35 mkazi wa Mtoni Mtongani jijini  Dar es salaam anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Mbeya kwa tuhuma za kutumia maneno ya kichochezi dhidi ya dini nyingine kuhubiri kanisani.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani mbeya Diwani Athumani, amesema mchungaji huyo alikamatwa Januari 30 mwaka huu, katika eneo la Iyunga nje ya Kanisa la Moravian ushirika wa Iyunga jijini Mbeya
Kamanda amesema uchochezi huo haukuwafurahisha baadhi ya waumini ambapo walitoa taarifa  polisi  na mchungaji huyo amekamatwa akiwa na cd na vipeperushi ambavyo ni sehemu ya uchunguzi unaoendelea
Aidha kamanda Athumani amewataka wananchi wote kuwachukia kutowakumbatia wachochezi wa madhehebu ya dini yoyote ili kujiepusha na madhara ambayo yamekuwa yakionekana katika baadhi ya maeneo nchini na duniani.
Hata hivyo ametoa pongezi kwa wote wanaoendelea kuthamini amani, usalama na utulivu hususani waumini waliotoa taarifa hiyo na kufanikisha kukamatwa muinjilisti huyo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI