NJIA ZA KILI MARATHON 2013 ZATAJWA
Waandaaji
wa Kilimanjaro Marathon 2013 wametangaza kwamba mbio za mwaka huu
zitafanyika katika njia zile zile zilizotumika mwaka jana. Mbio hizo
limepangwa kufanyika tarehe 3 Machi 2013 mjini Moshi.
John
Addison, Mkurugenzi Mtendaji wa Wild Frontiers, ambao ni waandaaji wa
tukio hilo alisema katika taarifa jana kwamba njia zitakazotumika kwa
ajili ya Kilimanjaro Marathon 2013 ni kuanzia Uwanja wa chuo cha
Ushirika (MUCCoBS) kuelekea katikati ya mji, na kisha kufuata barabara
kuu ya kwenda Dar -Es- Salaam kwa takriban kilomita 8 hadi 9, baadae
watageuka na kurudi Moshi mjini kupitia katikati ya mji, na badae
watapandisha mwinuko kidogo kuelekea Mweka, "wanariadha watafurahia
zaidi sehemu hii kwasababu ina mandhari ya kuvutia na kutakuwa na
washangiliaji wengi kandoAddison anasema “sehemu ya kupandisha kuelekea
Mweka inahitaji kupanda kwa taratibu lakini kwa sababu Mlima
Kilimanjaro ni kivutio na uwepo wa wananchi wanaoshangilia muda unaenda
haraka na kuwasaidia wakimbiaji kumaliza mapema. Alisema kuwa kituo cha
cha Mweka ambapo wanaridha wanageukia kurudi uwanja wa Ushirika inakuwa
ni takribani kilometa 32 tangu kuanza mbio ndefu ya kilomita 42. Baada
ya hapo kipande kilichobaki inakuwa ni mteremko kuelekea uwanjani mwisho
wa mbio na njia nzima ni mteremko tu.
Aliongeza
kuwa kwa wale watakaoshiriki nusu Marathon, mbio zitaanzia uwanja wa
MUCCoBS ambapo pako tambarare na baadae watapandisha kwenye mwinuko
kidogo kuelekea Mweka kama ilivyo zile mbio ndefu kabla ya kurudi umbali
wa takriban km 10, kuelekea tena uwanjani.
Kutakuwa
na meza za maji kama ilivyo kawaida na magari maalum ya kunyunyizia
maji mithili ya mvua kando ya barabara huduma ambazo zimeandaliwa maalum
kuwafanya wanariadha waendelee kuwa na nguvu wakati wote wa mbio hizo.
Kuhusu
burudani, Addison alisema kuwa hali ya uwanjani itakua ya kusisimua
kutokana na burudani kali kutoka bendi za muziki wa nyumbani
zitakazokuwepo, chakula cha kutosha, nyama choma na vinywaji na bila
kusahau mbio za kujifurahisha za Vodacom 5km Fun Run ambazo pia
zinatarajiwa kuleta msisimko wa aina yake.
“Ili
kuhakikisha usalama wa wakimbiaji, baadhi ya barabara zitakuwa
zimefungwa, asubuhi siku ya mbio, lakini kutakuwepo na njia mbadala
kuzunguka mji kwa ajili ya wakazi wa Moshi. Wakazi wa moshi ambao
wanatarajia kukimbia pamoja na wakimbiaji wengine watakaofika Moshi
mapema wanaweza kuanza mazoezi katika njia hizo hili kupata uzoefu wa
njia na kujiandaa vizuri kwa ajili ya mbio.
Mbio
hizo zinaratibiwa na Executive Solutions na kudhaminiwa na Kilimanjaro
PremiumLager, huku wadhamini wengine wa tukio hilo ni pamoja na Vodacom
Tanzania (5km Fun Run), GAPCO (Nusu Marathon Walemavu), Tanga Cement,
CFAO Motors, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, TanzaniteOne, New
Arusha Hoteli, Kilimanjaro Water, FastJet na Shirika la Umoja wa Mataifa
la Idadi ya Watu (UNFPA). ya barabara”.
Comments