POLISI TARAFA WATAKIWA KUTUMIA PIKIPIKI KWA MATUMIZI YALIYOKUSUDIWA


DSC_8334Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Stanslaus Mulongo amewataka Wakaguzi wa Polisi wa Tarafa kuzitumia pikipiki walizokabidhiwa kwa matumizi yaliyokusudiwa tena kwa hekima kubwa na si vinginevyo.
Hayo aliyasema jana katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa gwaride uliopo kwenye kambi mojawapo iliyopo mjini hapa ambapo jumla ya pikipiki 12 zilikabidhiwa kwa Wakuu wa Polisi wa wilaya za Mkoa huu ambao walipokea kwa niaba ya Wakaguzi hao.
Aliendelea kuwataka Wakaguzi hao kutumia vyombo hivyo vya usafiri kwa kuwahi katika maeneo yenye matatizo ya kiuhalifu na pia kuendelea kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali hali ambayo itasaidia kuzuia uhalifu.
Pia aliwaomba Watendaji wa Kata na Tarafa kuwapokea Wakaguzi hao kwa mikono miwili ili kurahisisha utendaji wa kazi za ulinzi katika maeneo yao.
“Wapokeeni hao wenzetu, wasaidieni kwani nyinyi mnajua mazingira vizuri hali ambayo itasaidia kupunguza uhalifu”. Alisisitiza Mh. Mulongo.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas, alisema kwamba pikipiki hizo zitawasaidia Wakaguzi hao kuwa karibu na wananchi kwa kutembelea kwenye maeneo mbalimbali ya Tarafa zao.
Kamanda Sabas alimalizia kwa kusema kwamba, sababu za kutolewa kwa pikipiki hizo ni kusaidia kupunguza uhalifu katika maeneo yao hali ambayo itasaidia jamii kukaa kwa usalama.
Jeshi la Polisi nchini lilitoa pikipiki hizo kwa Makamanda wa mikoa yote hapa nchini tarehe 11/01/2013 katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo huku Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dar es Salaam Naibu Kamishna Suleimani Kova akipokea pikipiki hizo kwa niaba ya Makamanda hao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.