Leo
tarehe 13 Februari 2013, Shirika la Nyumba la Taifa linapenda
kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa lipo katika mchakato wa kuboresha
mazingira upangaji na upangishaji na leo linataka kutoa taarifa kuu
mbili muhimu.
1. Kupangishana katika nyumba za Shirika bila Kibali (Illegal Subletting)
Mwaka
2010, Shirika liliwatangazia watu waliopangishwa kwenye nyumba za
Shirika kinyume cha taratibu wajitokeze ili waweze kupewa upangaji moja
kwa moja na Shirika. Baadhi yao walijitokeza na walipewa upangaji.
Hata
hivyo imeonekana kuna ambao hawakujitokeza kwasababu yoyote ile,
Shirika sasa linawatangazia tena wajitokeze ili waweze kuhalalishwa
ukaaji wao (kupewa upangaji wa Shirika). Wanaombwa kujitokeza ndani ya
kipindi cha miezi mitatu (kuanzia tarehe ya taarifa hii).
Baada ya hapo fursa ya kutambuliwa haitakuwapo tena, bali watatolewa kwenye nyumba hizo na zitapangishwa kwa watu wengine.
2. Uhuishaji wa mikataba ya upangaji (Lease Renewal)
Mwaka
2006 Shirika lilifanya uhakiki wa wapangaji pamoja na kutoa mikataba
mipya yenye muda maalumu baada ya kufuta ile iliyokuwa haina kikomo.
Imeonekana kuna wapangaji ambao hawakujitokeza kipindi hicho, wengine
waliopewa mikataba ya muda maalumu imeshakwisha muda wake.
Shirika
limefanya juhudi mbalimbali ikiwamo kuwaandikia barua za kuwakumbusha
kwenda ofisi za Shirika kuchukua mikataba, baadhi wamekwenda na wengine
hawajafanya hivyo na kubaki bila mikataba.
Shirika
linapenda ifahamike kuwa kwa mpangaji kutokuwa na mkataba kwasababu
yoyote ile ina maana kwamba hajakubaliana na masharti ya upangaji.
Shirika linatoa muda wa mwezi mmoja kuanzia tarehe ya taarifa hii kwa
yeyote ambaye mkataba wake umemaliza muda au hana mkataba afike ofisi za
Shirika ili aweze kupewa mkataba.
Shirika linapenda kusisitiza kuwa kutokufanya hivyo ndani ya kipindi cha mwezi mmoja uliotolewa
tachukuliwa kuwa ni ukiukaji wa masharti ya upangaji na baada ya hapo
wale wote ambao watakuwa hawana mikataba ya upangaji . Shirika
litalazimika kuwatoa kwenye nyumba kwani watakuwa wameonyesha kuwa
hawahitaji upangaji.
Shirika
pia linapenda ifahamike kuwa halina mikataba ambayo haina kikomo wala
mikataba ya mwezi kwa mwezi. Pia mkataba ili ukamilike lazima uwe
umesainiwa na pande zote mbili yaani Shirika la Nyumba na mpangaji
anayetambulika.
IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA
Comments