TRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA MASHINE ZA KODI (EFDs) KWA WAFANYABIASHARA WASIOSAJILIWA NA VAT MKOA WA ILALA
Ofisa wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa Mkoa wa Kodi wa Wilaya ya Ilala, George Haule, akitoa mada kwa wafanyabiashara wakati wa semina hiyo |
Baadhi ya Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini mwezeshaji wa semina semina hiyo Bw.George Haule. |
Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini mwezeshaji wa semina semina hiyo Bw.Hamisi Lupenja. |
Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini mwezeshaji wa semina hiyo. Bw.Hamisi Lupenja. |
Wafanyabiashara wakiwa katika semina hiyo.
Na Dotto Mwaibale
WAFANYABIASHA nchini wametakiwa kufungua namba ya mlipa kodi (TIN) ili watambulike na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Mwito huo umetolewa Dar es Salaam leo na Ofisa wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa Mkoa wa Kodi wa Wilaya ya Ilala, George Haule wakati akitoa mada katika semina ya siku moja kwa wafanyabiashara wa Kata ya Buguruni kuhusu matumizi ya mfumo wa mashine za kodi (EFDs) kwa wafanyabiashara wasiosajiliwa na VAT wa mkoa wa kodi wa Ilala.
Alisema ni muhimu kwa kila mfanyabiashara kuwa na namba hiyo ya utambuzi kwani itamuwezesha kutambulika na Mamlaka hiyo na itakuwa rahisi kujua kodi anayopaswa kulipa kutokana na biashara yake.
Mwezeshaji mwingine katika semina hiyo Ofisa Elimu na Huduma kwa mlipa kodi Kanda ya Mashariki Hamisi Lupenja alisema julai 1, 2010 serikali ilianzisha matumizi ya mashine hizo kwa wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT lengo likiwa ni kuleta uwiano katika ulipaji wa kodi.
Alisema wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT wataanza kutumia mashine hizo mwaka huu kwa sheria ya kodi ya mapato sura 332 na kanuni ya mwaka 2012 ndiyo itakayo tumika EFD.
Alisema kutambulika kwa mlipa kodi na kumbukumbu za mauzo yake inaisaidia mamlaka hiyo kujua kupanga kodi kwa mfanyabiashara husika tofauti na kwa mfanyabiashara ambaye hana kumbukumbu.
"Kuweka kumbukumbu za biashara katika kitabu inasaidia hata kwa mtu mwingine kujua mwenendo wa biashara iliyopo hata kama muhusika atakuwa amepata na matitizo ikiwemo kifo" alisema Lupenja.
Wafanyabaiashara hao walisema wamekuwa na changamoto kubwa ya kupangiwa kodi kubwa na mamlaka hiyo jambo linalowafanya washindwe kuendesha biashara zao.
Hata hivyo waliondolewa wasiwasi na Lupenja kwa kuwaambia mamlaka hiyo haimbambikii mfanyabiashara kodi kubwa na akatoa mwito kuwa wawe wazi katika biashara zao.
"Msiwaogope wafanyakazi wa TRA na kuwakwepa kutolipa kodi wanao waogopa ni wale wanaofanyabiashara zao kwa vificho kwani TRA ni rafiki ya ninyi wafanyabiashara" alisema Lupenja
WAFANYABIASHA nchini wametakiwa kufungua namba ya mlipa kodi (TIN) ili watambulike na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Mwito huo umetolewa Dar es Salaam leo na Ofisa wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa Mkoa wa Kodi wa Wilaya ya Ilala, George Haule wakati akitoa mada katika semina ya siku moja kwa wafanyabiashara wa Kata ya Buguruni kuhusu matumizi ya mfumo wa mashine za kodi (EFDs) kwa wafanyabiashara wasiosajiliwa na VAT wa mkoa wa kodi wa Ilala.
Alisema ni muhimu kwa kila mfanyabiashara kuwa na namba hiyo ya utambuzi kwani itamuwezesha kutambulika na Mamlaka hiyo na itakuwa rahisi kujua kodi anayopaswa kulipa kutokana na biashara yake.
Mwezeshaji mwingine katika semina hiyo Ofisa Elimu na Huduma kwa mlipa kodi Kanda ya Mashariki Hamisi Lupenja alisema julai 1, 2010 serikali ilianzisha matumizi ya mashine hizo kwa wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT lengo likiwa ni kuleta uwiano katika ulipaji wa kodi.
Alisema wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT wataanza kutumia mashine hizo mwaka huu kwa sheria ya kodi ya mapato sura 332 na kanuni ya mwaka 2012 ndiyo itakayo tumika EFD.
Alisema kutambulika kwa mlipa kodi na kumbukumbu za mauzo yake inaisaidia mamlaka hiyo kujua kupanga kodi kwa mfanyabiashara husika tofauti na kwa mfanyabiashara ambaye hana kumbukumbu.
"Kuweka kumbukumbu za biashara katika kitabu inasaidia hata kwa mtu mwingine kujua mwenendo wa biashara iliyopo hata kama muhusika atakuwa amepata na matitizo ikiwemo kifo" alisema Lupenja.
Wafanyabaiashara hao walisema wamekuwa na changamoto kubwa ya kupangiwa kodi kubwa na mamlaka hiyo jambo linalowafanya washindwe kuendesha biashara zao.
Hata hivyo waliondolewa wasiwasi na Lupenja kwa kuwaambia mamlaka hiyo haimbambikii mfanyabiashara kodi kubwa na akatoa mwito kuwa wawe wazi katika biashara zao.
"Msiwaogope wafanyakazi wa TRA na kuwakwepa kutolipa kodi wanao waogopa ni wale wanaofanyabiashara zao kwa vificho kwani TRA ni rafiki ya ninyi wafanyabiashara" alisema Lupenja
Comments