TRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA MASHINE ZA KODI (EFDs) KWA WAFANYABIASHARA WASIOSAJILIWA NA VAT MKOA WA ILALA

Ofisa Elimu na Huduma kwa mlipa kodi Kanda ya 
Mashariki wa Mamlaka ya  Mapato Tanzania (TRA), 
Hamisi Lupenja (kulia), akitoa mada katika semina ya 
siku moja kwa wafanyabiashara wa Kata ya Buguruni 
kuhusu matumizi ya mfumo wa mashine za kodi (EFDs) 
kwa wafanyabiashara wasiosajiliwa na VAT wa 
mkoa wa 
kodi wa Ilala. Semina hiyo imefanyika Dar es Salaam leo. 
(Picha habari na mwaibale.blogspot.com)
 Ofisa wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa Mkoa 
wa Kodi wa Wilaya ya Ilala, George Haule, akitoa 
mada kwa wafanyabiashara wakati wa semina hiyo
Baadhi ya Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini 
mwezeshaji wa semina semina hiyo Bw.George Haule.
Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini 
mwezeshaji wa semina semina hiyo Bw.Hamisi Lupenja.
Wafanyabiashara hao wakimsikiliza kwa makini 
mwezeshaji wa semina  hiyo. Bw.Hamisi Lupenja.
Wafanyabiashara wakiwa katika semina hiyo.
Na Dotto Mwaibale

WAFANYABIASHA nchini wametakiwa kufungua namba ya mlipa kodi (TIN) ili watambulike na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Mwito huo umetolewa Dar es Salaam leo na Ofisa wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa Mkoa wa Kodi wa Wilaya ya Ilala, George Haule wakati akitoa mada katika semina ya siku moja kwa wafanyabiashara wa Kata ya Buguruni kuhusu matumizi ya mfumo wa mashine za kodi (EFDs) kwa wafanyabiashara wasiosajiliwa na VAT wa mkoa wa kodi wa Ilala.

Alisema ni muhimu kwa kila mfanyabiashara kuwa na namba hiyo ya utambuzi kwani itamuwezesha kutambulika na Mamlaka hiyo na itakuwa rahisi kujua kodi anayopaswa kulipa kutokana na biashara yake.

Mwezeshaji mwingine katika semina hiyo Ofisa Elimu na Huduma kwa mlipa kodi Kanda ya Mashariki Hamisi Lupenja  alisema julai 1, 2010 serikali ilianzisha matumizi ya mashine hizo kwa wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT  lengo likiwa ni kuleta uwiano katika ulipaji wa kodi.

Alisema wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT wataanza kutumia mashine hizo mwaka huu kwa sheria ya kodi ya mapato sura 332 na kanuni ya  mwaka 2012 ndiyo itakayo tumika EFD.

Alisema kutambulika kwa mlipa kodi na kumbukumbu za mauzo yake inaisaidia mamlaka hiyo kujua kupanga kodi kwa mfanyabiashara husika tofauti na kwa mfanyabiashara ambaye hana kumbukumbu.

"Kuweka kumbukumbu za biashara katika kitabu inasaidia hata kwa mtu mwingine kujua mwenendo wa biashara iliyopo hata kama muhusika atakuwa amepata na matitizo ikiwemo kifo" alisema Lupenja.

Wafanyabaiashara hao walisema wamekuwa na changamoto kubwa ya kupangiwa kodi kubwa na mamlaka hiyo jambo linalowafanya washindwe kuendesha biashara zao.

Hata hivyo waliondolewa wasiwasi na Lupenja kwa kuwaambia mamlaka hiyo haimbambikii mfanyabiashara kodi kubwa na akatoa mwito kuwa wawe wazi katika biashara zao.

"Msiwaogope wafanyakazi wa TRA na kuwakwepa kutolipa kodi wanao waogopa ni wale wanaofanyabiashara zao kwa vificho kwani TRA ni rafiki ya ninyi wafanyabiashara" alisema Lupenja

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.