WANA-CCM WAMPONGEZA SILAA KUWA MJUMBE WA CC YA CCM

Baadhi ya kinamama wa Gongo la Mboto ambao ni wananchama wa CCM wakiwasili kwenye Uwanja uliopo karibu na reli Gongo la Mboto katika mkutano wa hadhara wa kumpongeza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto Jerry Silaa baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa. (Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog).
Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmshauri Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akisalimiana na waendesha Boda boda wa Gongo la Mboto waliofika kumlaki akitokea mjini Dodoma.
Msafara wa waendesha Boda boda ukimsindikiza Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa kwenye viwanja vya Gongo la Mboto alipoandaliwa sherehe ya kumpongeza iliyoenda sambamba na mkutano wa hadhara.
Watoto waliokuwa pembezoni mwa barabara wakimpungua kwa furaha Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa alipokuwa akipita na msafara wake.
Pichani Juu na Chini ni baadhi ya viongozi wa CCM wakimlaki Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa katika Ofisi za CCM kata ya Gongo la Mboto alipopita kutia baraka ofisi hizo akielekea kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa kwa ajili ya kumpongeza.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmshauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa akitia saini kitabu cha wageni cha Ofisi za CCM kata ya Gongo la Mboto.
Waendesha boda boda wa Gongo la Mboto wakitia mbwembwe katika mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza Jerry Silaa aliyeteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Msafara wa Jerry Silaa ukiwasili uwanjani hapo kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Gongo la Mboto.
Mjumbe wa kamati kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa akipunga mkono kwa wananchi, WanaCCM waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza kuchaguliwa nafasi nyeti ya Chama cha Mapinduzi.
Mjumbe wa Kamati kuu na Halmashauri kuu ya CCM taifa Jerry Silaa akivishwa skafu ya chama mara baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Gongo la Mboto.
Jerry Silaa akivishwa lubega ya kimasai baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana Gongo la Mboto jijini Dar.
Pichani juu na chini ni Baadhi WanaCCM wa kata ya Gongo la Mboto wakimpongeza Jerry Silaa baada ya kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati kuu na Halmashauri kuu ya CCM Taifa wakati wa mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza katika viwanja vya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya umati wa wakazi wa Gongo la Mboto wakubwa kwa wadogo waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza Jerry Silaa.
Wanenguaji wa Mashujaa Band wakicheza staili ya Boda boda na Wana CCM wa Gongo la Mboto wakati wa mkutano wa hadhara.
"UTU UZIMA DAWA KWA RAHA ZETU"...Rappa wa Bendi ya Mashujaa akicheza sambamba na kinamama wa Kata ya Gongo la Mboto wakati wa sherehe za kumpongeza Jerry Silaa zilizoenda sambamba na mkutano wa hadhara.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*