WANA-CCM WAMPONGEZA SILAA KUWA MJUMBE WA CC YA CCM
Baadhi ya kinamama wa
Gongo la Mboto ambao ni wananchama wa CCM wakiwasili kwenye Uwanja
uliopo karibu na reli Gongo la Mboto katika mkutano wa hadhara wa
kumpongeza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa
Kata ya Gongo la Mboto Jerry Silaa baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mjumbe wa
Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa. (Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog).
Mjumbe wa Kamati Kuu na
Halmshauri Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Mstahiki Meya Manispaa ya
Ilala Jerry Silaa akisalimiana na waendesha Boda boda wa Gongo la Mboto
waliofika kumlaki akitokea mjini Dodoma.
Msafara wa waendesha
Boda boda ukimsindikiza Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM
Taifa Jerry Silaa kwenye viwanja vya Gongo la Mboto alipoandaliwa
sherehe ya kumpongeza iliyoenda sambamba na mkutano wa hadhara.
Watoto waliokuwa
pembezoni mwa barabara wakimpungua kwa furaha Mjumbe wa Kamati Kuu na
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa alipokuwa akipita na msafara
wake.
Pichani Juu na Chini ni
baadhi ya viongozi wa CCM wakimlaki Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri
Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa katika Ofisi za CCM kata ya Gongo la Mboto
alipopita kutia baraka ofisi hizo akielekea kwenye mkutano wa hadhara
ulioandaliwa kwa ajili ya kumpongeza.
Mstahiki Meya wa
Manispaa ya Ilala na Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto ambaye pia ni
Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmshauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa akitia
saini kitabu cha wageni cha Ofisi za CCM kata ya Gongo la Mboto.
Waendesha boda boda wa
Gongo la Mboto wakitia mbwembwe katika mkutano wa hadhara ulioenda
sambamba na sherehe za kumpongeza Jerry Silaa aliyeteuliwa kuwa Mjumbe
wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mh. Rais Jakaya Mrisho
Kikwete.
Msafara wa Jerry Silaa ukiwasili uwanjani hapo kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Gongo la Mboto.
Mjumbe wa kamati kuu na
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jerry Silaa akipunga mkono kwa wananchi,
WanaCCM waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na
sherehe za kumpongeza kuchaguliwa nafasi nyeti ya Chama cha Mapinduzi.
Mjumbe wa Kamati kuu na
Halmashauri kuu ya CCM taifa Jerry Silaa akivishwa skafu ya chama mara
baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja
vya Gongo la Mboto.
Jerry Silaa akivishwa lubega ya kimasai baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana Gongo la Mboto jijini Dar.
Pichani juu na chini ni
Baadhi WanaCCM wa kata ya Gongo la Mboto wakimpongeza Jerry Silaa baada
ya kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati kuu na Halmashauri kuu ya CCM Taifa
wakati wa mkutano wa hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza
katika viwanja vya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya umati wa
wakazi wa Gongo la Mboto wakubwa kwa wadogo waliohudhuria mkutano wa
hadhara ulioenda sambamba na sherehe za kumpongeza Jerry Silaa.
Wanenguaji wa Mashujaa Band wakicheza staili ya Boda boda na Wana CCM wa Gongo la Mboto wakati wa mkutano wa hadhara.
"UTU UZIMA DAWA KWA
RAHA ZETU"...Rappa wa Bendi ya Mashujaa akicheza sambamba na kinamama wa
Kata ya Gongo la Mboto wakati wa sherehe za kumpongeza Jerry Silaa
zilizoenda sambamba na mkutano wa hadhara.
Comments