Moja ya vazi la kanga lililobuniwa na Chichia. Picha ya Urban Pulse
Moja ya Ubunifu wa Anna Luks. Picha na Urban Pulse
Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe akiwa na mwanamuziki Freddy Macha aliyetumbuiza shughuli hii na gitaa lake. Picha na Fred Mchaki
Anna Luks na Christine Mhando. Picha ya Urban Pulse
Moja ya ubunifu wa Jacquiline Kibacha uliohamasishwa na jadi ya Wamasai. Picha ya F. Macha
Jacquiline Kibacha akipokea tuzo ya mapambo iitwayo “Fashions Finest 2012” mjini London mwezi Novemba mwaka jana. Picha na Simon Klyne

Jacquiline Kibacha anayetumia jina la Heart 365. Picha na F. Macha
Toka kulia, Mama Balozi- Joyce Kallaghe, Anna Lukindo, Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe, Christine Mhando, Naibu Balozi Chabaka Kilumanga na mkewe Irene. Picha na Urban Pulse
Naibu Balozi na mkewe Irene, Aruna Mbeyu, Chichia London, Balozi P Kallaghe, Anna Luks, Mariam Mungula wa CCM Barking. Picha na Fred Mchaki.
Mshoni Christine Mhando (Chichia London) akiongea na baadhi ya wageni. Picha na Urban Pulse
Anna Luks, Mama Mhando na Chichia. Picha ya Urban Pulse
Wageni wa Kijapani wakiwa na Chichia anayehamasisha fani ya Khanga. Picha na Aaron Miclat.
Marim Mungula, Baraka Baraka, Anna Luks, Wilkins Kiondo, Chichia, Samson Soboye. Picha na Fred Mchaki.
---
Imeandikwa na Kuletwa hapa Hakingowi.com na Freddy Macha

Picha za Urban Pulse na F. Mchaki

Maonyesho maarufu ya mavazi –London Fashion Week- yaliyoanza rasmi Ijumaa iliyopita mjini London yameiweka ramani ya Tanzania duniani.

Shughuli hii muhimu kiuchumi na kisanaa inayoendelea juma zima na kuhusisha vituo vya kitamaduni na balozi 27 ina lengo la kutangaza vipaji vya wabunifu mavazi toka nchi zisizojulikana uwanja huu mahiri wa kimataifa unaosifika takriban miaka 30 sasa.
“London Fashion Week” ni moja ya maonyesho manne ulimwenguni yaliyoasisiwa rasmi kutukuza ubunifu, ufundi na biashara mwaka 1984. Huendeshwa sambamba miji ya New York, Milan na Paris kila mwezi Februari na Septemba.

Watanzania tulioingia kwa dhamira ya “Swahili Flavour” (Ladha ya Kiswahili) tumefadhiliwa na Ubalozi wa Tanzania London ukishirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB). Watayarishaji wa shughuli hii ni shirika la kitamaduni na elimu Uingereza- British Council lenye mahusiano ya kirafiki na nchi 100 duniani.

“Maonyesho ya mavazi London ni fani ya hali ya juu na kibiashara ambapo waume kwa wanawake huwa pamoja wakibadilishana mapambo na visaidizi vyake,” anasema Julian Roberts, mbunifu mavazi wa British Council.

Akiongea rasmi kwenye ufunguzi wa Ijumaa uliokuwa na vinywaji baridi na muziki wa Kiswahili, mke wa Balozi Uingereza, Mama Joyce Kallaghe aliwasifu wabunifu mavazi wetu na kuwakabirisha wageni mbalimbali waliohudhuria “kuzitembelea mbuga nzuri za Kitanzania kama watafurahishwa na mavazi na ladha yetu ya Kiswahili.”

Wabunifu na washoni hao watatu ni Christine Mhando ( “Chichia London”), Anna Lukindo ( “Anna Luks”) na Jacquleine Kibacha (“Heart 365”). Kibacha ambaye pia ni mtunzi wa mashairi huchanganya desturi za kijadi na kisasa kwa shanga shanga, manyoya ya ndege na mapambo yaliyotokana na sanaa za Wamasai. Miezi mitatu iliyopita kazi zake Kibacha zilipata tuzo maarufu la “Fashions Finest 2012.”

Akifafanua fani yake, Christine “Chichia” Mhando aliyehitimu chuo cha Usanii cha Kent mwaka 2002 alisema yeye huhamasisha vazi la Kanga, misemo na maneno ya Kiswahili mathalan “Tongoza”, “Ala Kumbe!” na “Zungumza” kama wajihi wa kazi hiyo. Anna Luks aliyefuzu shahada ya mwanzo (BA) chuo cha Middlesex, alieleza azma yake ni kumwonyesha mwanamke wa Kitanzania alivyo kupitia mitindo kama “dunia pana” , “kaba roho” na “baibui.” Anna Luks huchanganya ushonaji wa mikono, kamba kamba na mavazi ya kisasa.

Naibu Balozi, Mheshimiwa Chabaka Kilumanga alisema maonyesho haya ya kimataifa yatakua nafasi kubwa kwa Tanzania kujitangaza kibiashara na ni sehemu mahsusi ya fahari ya utamaduni wetu.

Wahusika wengine waliochangia mafanikio ya shughuli ni Mratibu Ubalozini, Bi Rose Kiondo; Afisa mwangalizi wa onyesho hilo, Samson Soboye na Meneja wa dhana ya Swahili Flavour, Mike Puplampu.

Habari zilizopatikana jana zilisema kwamba wabunifu mavazi wa Kitanzania wametajwa ndani ya kundi la washindi kumi bora. Ushindi huo unathibitisha dhahiri uwezo wa sanaa na ubunifu wetu ndani ya hulka ya mavazi ya kimataifa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.